Sura zote

Surah 96

The Clot

سُورَةُ العَلَقِ

Al-Alaq · Makka

Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia

Sauti
  1. 1

    بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ ٱقْرَأْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلَّذِى خَلَقَ

    Unukuzi: Iqra bismi rab bikal lazee khalaq

    Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba,

  2. 2

    خَلَقَ ٱلْإِنسَٰنَ مِنْ عَلَقٍ

    Unukuzi: Khalaqal insaana min 'alaq

    Amemuumba binaadamu kwa tone la damu,

  3. 3

    ٱقْرَأْ وَرَبُّكَ ٱلْأَكْرَمُ

    Unukuzi: Iqra wa rab bukal akram

    Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote!

  4. 4

    ٱلَّذِى عَلَّمَ بِٱلْقَلَمِ

    Unukuzi: Al lazee 'allama bil qalam

    Ambaye amefundisha kwa kalamu.

  5. 5

    عَلَّمَ ٱلْإِنسَٰنَ مَا لَمْ يَعْلَمْ

    Unukuzi: 'Al lamal insaana ma lam y'alam

    Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui.

  6. 6

    كَلَّآ إِنَّ ٱلْإِنسَٰنَ لَيَطْغَىٰٓ

    Unukuzi: Kallaa innal insaana layatghaa

    Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri

  7. 7

    أَن رَّءَاهُ ٱسْتَغْنَىٰٓ

    Unukuzi: Ar-ra aahus taghnaa

    Akijiona katajirika.

  8. 8

    إِنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ ٱلرُّجْعَىٰٓ

    Unukuzi: Innna ilaa rabbikar ruj'aa

    Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo.

  9. 9

    أَرَءَيْتَ ٱلَّذِى يَنْهَىٰ

    Unukuzi: Ara-aital lazee yanhaa

    Umemwona yule anaye mkataza

  10. 10

    عَبْدًا إِذَا صَلَّىٰٓ

    Unukuzi: 'Abdan iza sallaa

    Mja anapo sali?

  11. 11

    أَرَءَيْتَ إِن كَانَ عَلَى ٱلْهُدَىٰٓ

    Unukuzi: Ara-aita in kana 'alal hudaa

    Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu?

  12. 12

    أَوْ أَمَرَ بِٱلتَّقْوَىٰٓ

    Unukuzi: Au amara bit taqwaa

    Au anaamrisha uchamngu?

  13. 13

    أَرَءَيْتَ إِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰٓ

    Unukuzi: Ara-aita in kaz zaba wa ta walla

    Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma?

  14. 14

    أَلَمْ يَعْلَم بِأَنَّ ٱللَّهَ يَرَىٰ

    Unukuzi: Alam y'alam bi-an nal lahaa yaraa

    Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona?

  15. 15

    كَلَّا لَئِن لَّمْ يَنتَهِ لَنَسْفَعًۢا بِٱلنَّاصِيَةِ

    Unukuzi: Kalla la illam yantahi la nasfa'am bin nasiyah

    Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele!

  16. 16

    نَاصِيَةٍۢ كَٰذِبَةٍ خَاطِئَةٍۢ

    Unukuzi: Nasiyatin kazi batin khaatiyah

    Shungi la uwongo, lenye makosa!

  17. 17

    فَلْيَدْعُ نَادِيَهُۥ

    Unukuzi: Fal yad'u naadiyah

    Basi na awaite wenzake!

  18. 18

    سَنَدْعُ ٱلزَّبَانِيَةَ

    Unukuzi: Sanad 'uz zabaaniyah

    Nasi tutawaita Mazabania!

  19. 19

    كَلَّا لَا تُطِعْهُ وَٱسْجُدْ وَٱقْتَرِب ۩

    Unukuzi: Kalla; la tuti'hu wasjud waqtarib

    Hasha! Usimt'ii! Nawe sujudu na ujongee!

Toleo la tafsiri: sw.barwani

Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).

Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.

Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.