Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia
- 1
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ ٱقْرَأْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلَّذِى خَلَقَ
Unukuzi: Iqra bismi rab bikal lazee khalaq
Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba,
- 2
خَلَقَ ٱلْإِنسَٰنَ مِنْ عَلَقٍ
Unukuzi: Khalaqal insaana min 'alaq
Amemuumba binaadamu kwa tone la damu,
- 3
ٱقْرَأْ وَرَبُّكَ ٱلْأَكْرَمُ
Unukuzi: Iqra wa rab bukal akram
Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote!
- 4
ٱلَّذِى عَلَّمَ بِٱلْقَلَمِ
Unukuzi: Al lazee 'allama bil qalam
Ambaye amefundisha kwa kalamu.
- 5
عَلَّمَ ٱلْإِنسَٰنَ مَا لَمْ يَعْلَمْ
Unukuzi: 'Al lamal insaana ma lam y'alam
Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui.
- 6
كَلَّآ إِنَّ ٱلْإِنسَٰنَ لَيَطْغَىٰٓ
Unukuzi: Kallaa innal insaana layatghaa
Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri
- 7
أَن رَّءَاهُ ٱسْتَغْنَىٰٓ
Unukuzi: Ar-ra aahus taghnaa
Akijiona katajirika.
- 8
إِنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ ٱلرُّجْعَىٰٓ
Unukuzi: Innna ilaa rabbikar ruj'aa
Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo.
- 9
أَرَءَيْتَ ٱلَّذِى يَنْهَىٰ
Unukuzi: Ara-aital lazee yanhaa
Umemwona yule anaye mkataza
- 10
عَبْدًا إِذَا صَلَّىٰٓ
Unukuzi: 'Abdan iza sallaa
Mja anapo sali?
- 11
أَرَءَيْتَ إِن كَانَ عَلَى ٱلْهُدَىٰٓ
Unukuzi: Ara-aita in kana 'alal hudaa
Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu?
- 12
أَوْ أَمَرَ بِٱلتَّقْوَىٰٓ
Unukuzi: Au amara bit taqwaa
Au anaamrisha uchamngu?
- 13
أَرَءَيْتَ إِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰٓ
Unukuzi: Ara-aita in kaz zaba wa ta walla
Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma?
- 14
أَلَمْ يَعْلَم بِأَنَّ ٱللَّهَ يَرَىٰ
Unukuzi: Alam y'alam bi-an nal lahaa yaraa
Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona?
- 15
كَلَّا لَئِن لَّمْ يَنتَهِ لَنَسْفَعًۢا بِٱلنَّاصِيَةِ
Unukuzi: Kalla la illam yantahi la nasfa'am bin nasiyah
Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele!
- 16
نَاصِيَةٍۢ كَٰذِبَةٍ خَاطِئَةٍۢ
Unukuzi: Nasiyatin kazi batin khaatiyah
Shungi la uwongo, lenye makosa!
- 17
فَلْيَدْعُ نَادِيَهُۥ
Unukuzi: Fal yad'u naadiyah
Basi na awaite wenzake!
- 18
سَنَدْعُ ٱلزَّبَانِيَةَ
Unukuzi: Sanad 'uz zabaaniyah
Nasi tutawaita Mazabania!
- 19
كَلَّا لَا تُطِعْهُ وَٱسْجُدْ وَٱقْتَرِب ۩
Unukuzi: Kalla; la tuti'hu wasjud waqtarib
Hasha! Usimt'ii! Nawe sujudu na ujongee!
Toleo la tafsiri: sw.barwani
Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).
Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.
Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.