Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia
- 1
بِّسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ إِنَّآ أَنزَلْنَٰهُ فِى لَيْلَةِ ٱلْقَدْرِ
Unukuzi: Innaa anzalnaahu fee lailatil qadr
Hakika Sisi tumeiteremsha Qur'ani katika Laylatul Qadri, Usiku wa Cheo Kitukufu.
- 2
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا لَيْلَةُ ٱلْقَدْرِ
Unukuzi: Wa maa adraaka ma lailatul qadr
Na nini kitacho kujuulisha nini Laylatul Qadri?
- 3
لَيْلَةُ ٱلْقَدْرِ خَيْرٌۭ مِّنْ أَلْفِ شَهْرٍۢ
Unukuzi: Lailatul qadri khairum min alfee shahr
Laylatul Qadri ni bora kuliko miezi elfu.
- 4
تَنَزَّلُ ٱلْمَلَٰٓئِكَةُ وَٱلرُّوحُ فِيهَا بِإِذْنِ رَبِّهِم مِّن كُلِّ أَمْرٍۢ
Unukuzi: Tanaz zalul malaa-ikatu war roohu feeha bi izni-rab bihim min kulli amr
Huteremka Malaika na Roho katika usiku huo kwa idhini ya Mola wao Mlezi kwa kila jambo.
- 5
سَلَٰمٌ هِىَ حَتَّىٰ مَطْلَعِ ٱلْفَجْرِ
Unukuzi: Salaamun hiya hattaa mat la'il fajr
Amani usiku huo mpaka mapambazuko ya alfajiri.
Toleo la tafsiri: sw.barwani
Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).
Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.
Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.