Sura zote

Surah 95

The Fig

سُورَةُ التِّينِ

At-Tin · Makka

Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia

Sauti
  1. 1

    بِّسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَٱلتِّينِ وَٱلزَّيْتُونِ

    Unukuzi: Wat teeni waz zaitoon

    Naapa kwa tini na zaituni!

  2. 2

    وَطُورِ سِينِينَ

    Unukuzi: Wa toori sineen

    Na kwa Mlima wa Sinai!

  3. 3

    وَهَٰذَا ٱلْبَلَدِ ٱلْأَمِينِ

    Unukuzi: Wa haazal balad-il ameen

    Na kwa mji huu wenye amani!

  4. 4

    لَقَدْ خَلَقْنَا ٱلْإِنسَٰنَ فِىٓ أَحْسَنِ تَقْوِيمٍۢ

    Unukuzi: Laqad khalaqnal insaana fee ahsani taqweem

    Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa.

  5. 5

    ثُمَّ رَدَدْنَٰهُ أَسْفَلَ سَٰفِلِينَ

    Unukuzi: Thumma ra dad naahu asfala saafileen

    Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini!

  6. 6

    إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّٰلِحَٰتِ فَلَهُمْ أَجْرٌ غَيْرُ مَمْنُونٍۢ

    Unukuzi: Ill-lal lazeena aamanoo wa 'amilus saalihaati; falahum ajrun ghairu mamnoon

    Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira usio kwisha.

  7. 7

    فَمَا يُكَذِّبُكَ بَعْدُ بِٱلدِّينِ

    Unukuzi: Fama yu kaz zibuka b'adu bid deen

    Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo?

  8. 8

    أَلَيْسَ ٱللَّهُ بِأَحْكَمِ ٱلْحَٰكِمِينَ

    Unukuzi: Alai sal laahu bi-ahkamil haakimeen

    Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu wote?

Toleo la tafsiri: sw.barwani

Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).

Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.

Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.

The Fig — Islam Word