Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia
- 1
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ أَلَمْ نَشْرَحْ لَكَ صَدْرَكَ
Unukuzi: Alam nashrah laka sadrak
Hatukukunjulia kifua chako?
- 2
وَوَضَعْنَا عَنكَ وِزْرَكَ
Unukuzi: Wa wa d'ana 'anka wizrak
Na tukakuondolea mzigo wako,
- 3
ٱلَّذِىٓ أَنقَضَ ظَهْرَكَ
Unukuzi: Allazee anqada zahrak
Ulio vunja mgongo wako?
- 4
وَرَفَعْنَا لَكَ ذِكْرَكَ
Unukuzi: Wa raf 'ana laka zikrak
Na tukakunyanyulia utajo wako?
- 5
فَإِنَّ مَعَ ٱلْعُسْرِ يُسْرًا
Unukuzi: Fa inna ma'al usri yusra
Basi kwa hakika pamoja na uzito upo wepesi,
- 6
إِنَّ مَعَ ٱلْعُسْرِ يُسْرًۭا
Unukuzi: Inna ma'al 'usri yusra
Hakika pamoja na uzito upo wepesi.
- 7
فَإِذَا فَرَغْتَ فَٱنصَبْ
Unukuzi: Fa iza faragh ta fansab
Na ukipata faragha, fanya juhudi.
- 8
وَإِلَىٰ رَبِّكَ فَٱرْغَب
Unukuzi: Wa ilaa rabbika far ghab
Na Mola wako Mlezi ndio mshughulikie.
Toleo la tafsiri: sw.barwani
Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).
Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.
Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.