Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia
- 1
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَٱلضُّحَىٰ
Unukuzi: Wad duhaa
Naapa kwa mchana!
- 2
وَٱلَّيْلِ إِذَا سَجَىٰ
Unukuzi: Wal laili iza sajaa
Na kwa usiku unapo tanda!
- 3
مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ
Unukuzi: Ma wad da'aka rabbuka wa ma qalaa
Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.
- 4
وَلَلْءَاخِرَةُ خَيْرٌۭ لَّكَ مِنَ ٱلْأُولَىٰ
Unukuzi: Walal-aakhiratu khairul laka minal-oola
Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.
- 5
وَلَسَوْفَ يُعْطِيكَ رَبُّكَ فَتَرْضَىٰٓ
Unukuzi: Wa la sawfa y'uteeka rabbuka fatarda
Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.
- 6
أَلَمْ يَجِدْكَ يَتِيمًۭا فَـَٔاوَىٰ
Unukuzi: Alam ya jidka yateeman fa aawaa
Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?
- 7
وَوَجَدَكَ ضَآلًّۭا فَهَدَىٰ
Unukuzi: Wa wa jadaka daal lan fahada
Na akakukuta umepotea akakuongoa?
- 8
وَوَجَدَكَ عَآئِلًۭا فَأَغْنَىٰ
Unukuzi: Wa wa jadaka 'aa-ilan fa aghnaa
Akakukuta mhitaji akakutosheleza?
- 9
فَأَمَّا ٱلْيَتِيمَ فَلَا تَقْهَرْ
Unukuzi: Fa am mal yateema fala taqhar
Basi yatima usimwonee!
- 10
وَأَمَّا ٱلسَّآئِلَ فَلَا تَنْهَرْ
Unukuzi: Wa am mas saa-ila fala tanhar
Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!
- 11
وَأَمَّا بِنِعْمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثْ
Unukuzi: Wa amma bi ni'mati rabbika fahad dith
Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.
Toleo la tafsiri: sw.barwani
Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).
Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.
Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.