Sura zote

Surah 93

The Morning Hours

سُورَةُ الضُّحَىٰ

Ad-Dhuhaa · Makka

Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia

Sauti
  1. 1

    بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَٱلضُّحَىٰ

    Unukuzi: Wad duhaa

    Naapa kwa mchana!

  2. 2

    وَٱلَّيْلِ إِذَا سَجَىٰ

    Unukuzi: Wal laili iza sajaa

    Na kwa usiku unapo tanda!

  3. 3

    مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ

    Unukuzi: Ma wad da'aka rabbuka wa ma qalaa

    Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.

  4. 4

    وَلَلْءَاخِرَةُ خَيْرٌۭ لَّكَ مِنَ ٱلْأُولَىٰ

    Unukuzi: Walal-aakhiratu khairul laka minal-oola

    Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.

  5. 5

    وَلَسَوْفَ يُعْطِيكَ رَبُّكَ فَتَرْضَىٰٓ

    Unukuzi: Wa la sawfa y'uteeka rabbuka fatarda

    Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.

  6. 6

    أَلَمْ يَجِدْكَ يَتِيمًۭا فَـَٔاوَىٰ

    Unukuzi: Alam ya jidka yateeman fa aawaa

    Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?

  7. 7

    وَوَجَدَكَ ضَآلًّۭا فَهَدَىٰ

    Unukuzi: Wa wa jadaka daal lan fahada

    Na akakukuta umepotea akakuongoa?

  8. 8

    وَوَجَدَكَ عَآئِلًۭا فَأَغْنَىٰ

    Unukuzi: Wa wa jadaka 'aa-ilan fa aghnaa

    Akakukuta mhitaji akakutosheleza?

  9. 9

    فَأَمَّا ٱلْيَتِيمَ فَلَا تَقْهَرْ

    Unukuzi: Fa am mal yateema fala taqhar

    Basi yatima usimwonee!

  10. 10

    وَأَمَّا ٱلسَّآئِلَ فَلَا تَنْهَرْ

    Unukuzi: Wa am mas saa-ila fala tanhar

    Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!

  11. 11

    وَأَمَّا بِنِعْمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثْ

    Unukuzi: Wa amma bi ni'mati rabbika fahad dith

    Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.

Toleo la tafsiri: sw.barwani

Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).

Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.

Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.