Sura zote

Surah 92

The Night

سُورَةُ اللَّيۡلِ

Al-Lail · Makka

Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia

Sauti
  1. 1

    بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَٱلَّيْلِ إِذَا يَغْشَىٰ

    Unukuzi: Wallaili izaa yaghshaa

    Naapa kwa usiku unapo funika!

  2. 2

    وَٱلنَّهَارِ إِذَا تَجَلَّىٰ

    Unukuzi: Wannahaari izaa tajalla

    Na mchana unapo dhihiri!

  3. 3

    وَمَا خَلَقَ ٱلذَّكَرَ وَٱلْأُنثَىٰٓ

    Unukuzi: Wa maa khalaqaz zakara wal unthaa

    Na kwa Aliye umba dume na jike!

  4. 4

    إِنَّ سَعْيَكُمْ لَشَتَّىٰ

    Unukuzi: Inna sa'yakum lashattaa

    Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali.

  5. 5

    فَأَمَّا مَنْ أَعْطَىٰ وَٱتَّقَىٰ

    Unukuzi: Fa ammaa man a'taa wattaqaa

    Ama mwenye kutoa na akamchamngu,

  6. 6

    وَصَدَّقَ بِٱلْحُسْنَىٰ

    Unukuzi: Wa saddaqa bil husnaa

    Na akaliwafiki lilio jema,

  7. 7

    فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلْيُسْرَىٰ

    Unukuzi: Fasanu yassiruhoo lilyusraa

    Tutamsahilishia yawe mepesi.

  8. 8

    وَأَمَّا مَنۢ بَخِلَ وَٱسْتَغْنَىٰ

    Unukuzi: Wa ammaa mam bakhila wastaghnaa

    Na ama mwenye kufanya ubakhili, na asiwe na haja ya wenzake,

  9. 9

    وَكَذَّبَ بِٱلْحُسْنَىٰ

    Unukuzi: Wa kazzaba bil husnaa

    Na akakanusha lilio jema,

  10. 10

    فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلْعُسْرَىٰ

    Unukuzi: Fasanu yassiruhoo lil'usraa

    Tutamsahilishia yawe mazito!

  11. 11

    وَمَا يُغْنِى عَنْهُ مَالُهُۥٓ إِذَا تَرَدَّىٰٓ

    Unukuzi: Wa maa yughnee 'anhu maaluhooo izaa taraddaa

    Na mali yake yatamfaa nini atapo kuwa anadidimia?

  12. 12

    إِنَّ عَلَيْنَا لَلْهُدَىٰ

    Unukuzi: Inna 'alainaa lal hudaa

    Hakika ni juu yetu kuonyesha uwongofu.

  13. 13

    وَإِنَّ لَنَا لَلْءَاخِرَةَ وَٱلْأُولَىٰ

    Unukuzi: Wa inna lanaa lal Aakhirata wal oolaa

    Na hakika ni yetu Sisi Akhera na dunia.

  14. 14

    فَأَنذَرْتُكُمْ نَارًۭا تَلَظَّىٰ

    Unukuzi: Fa anzartukum naaran talazzaa

    Basi nakuonyeni na Moto unao waka!

  15. 15

    لَا يَصْلَىٰهَآ إِلَّا ٱلْأَشْقَى

    Unukuzi: Laa yaslaahaaa illal ashqaa

    Hatauingia ila mwovu kabisa!

  16. 16

    ٱلَّذِى كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ

    Unukuzi: Allazee kazzaba wa tawallaa

    Anaye kadhibisha na kupa mgongo.

  17. 17

    وَسَيُجَنَّبُهَا ٱلْأَتْقَى

    Unukuzi: Wa sa yujannnabuhal atqaa

    Na mchamngu ataepushwa nao,

  18. 18

    ٱلَّذِى يُؤْتِى مَالَهُۥ يَتَزَكَّىٰ

    Unukuzi: Allazee yu'tee maalahoo yatazakkaa

    Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa.

  19. 19

    وَمَا لِأَحَدٍ عِندَهُۥ مِن نِّعْمَةٍۢ تُجْزَىٰٓ

    Unukuzi: Wa maa li ahadin 'indahoo min ni'matin tujzaaa

    Na wala si kwa kuwa yupo yeyote aliye mfanyia hisani ndio anamlipa.

  20. 20

    إِلَّا ٱبْتِغَآءَ وَجْهِ رَبِّهِ ٱلْأَعْلَىٰ

    Unukuzi: Illab tighaaa'a wajhi rabbihil a 'laa

    Ila ni kutaka radhi ya Mola wake Mlezi aliye juu kabisa.

  21. 21

    وَلَسَوْفَ يَرْضَىٰ

    Unukuzi: Wa lasawfa yardaa

    Naye atakuja ridhika!

Toleo la tafsiri: sw.barwani

Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).

Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.

Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.

The Night — Islam Word