Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia
- 1
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَٱلَّيْلِ إِذَا يَغْشَىٰ
Unukuzi: Wallaili izaa yaghshaa
Naapa kwa usiku unapo funika!
- 2
وَٱلنَّهَارِ إِذَا تَجَلَّىٰ
Unukuzi: Wannahaari izaa tajalla
Na mchana unapo dhihiri!
- 3
وَمَا خَلَقَ ٱلذَّكَرَ وَٱلْأُنثَىٰٓ
Unukuzi: Wa maa khalaqaz zakara wal unthaa
Na kwa Aliye umba dume na jike!
- 4
إِنَّ سَعْيَكُمْ لَشَتَّىٰ
Unukuzi: Inna sa'yakum lashattaa
Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali.
- 5
فَأَمَّا مَنْ أَعْطَىٰ وَٱتَّقَىٰ
Unukuzi: Fa ammaa man a'taa wattaqaa
Ama mwenye kutoa na akamchamngu,
- 6
وَصَدَّقَ بِٱلْحُسْنَىٰ
Unukuzi: Wa saddaqa bil husnaa
Na akaliwafiki lilio jema,
- 7
فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلْيُسْرَىٰ
Unukuzi: Fasanu yassiruhoo lilyusraa
Tutamsahilishia yawe mepesi.
- 8
وَأَمَّا مَنۢ بَخِلَ وَٱسْتَغْنَىٰ
Unukuzi: Wa ammaa mam bakhila wastaghnaa
Na ama mwenye kufanya ubakhili, na asiwe na haja ya wenzake,
- 9
وَكَذَّبَ بِٱلْحُسْنَىٰ
Unukuzi: Wa kazzaba bil husnaa
Na akakanusha lilio jema,
- 10
فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلْعُسْرَىٰ
Unukuzi: Fasanu yassiruhoo lil'usraa
Tutamsahilishia yawe mazito!
- 11
وَمَا يُغْنِى عَنْهُ مَالُهُۥٓ إِذَا تَرَدَّىٰٓ
Unukuzi: Wa maa yughnee 'anhu maaluhooo izaa taraddaa
Na mali yake yatamfaa nini atapo kuwa anadidimia?
- 12
إِنَّ عَلَيْنَا لَلْهُدَىٰ
Unukuzi: Inna 'alainaa lal hudaa
Hakika ni juu yetu kuonyesha uwongofu.
- 13
وَإِنَّ لَنَا لَلْءَاخِرَةَ وَٱلْأُولَىٰ
Unukuzi: Wa inna lanaa lal Aakhirata wal oolaa
Na hakika ni yetu Sisi Akhera na dunia.
- 14
فَأَنذَرْتُكُمْ نَارًۭا تَلَظَّىٰ
Unukuzi: Fa anzartukum naaran talazzaa
Basi nakuonyeni na Moto unao waka!
- 15
لَا يَصْلَىٰهَآ إِلَّا ٱلْأَشْقَى
Unukuzi: Laa yaslaahaaa illal ashqaa
Hatauingia ila mwovu kabisa!
- 16
ٱلَّذِى كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ
Unukuzi: Allazee kazzaba wa tawallaa
Anaye kadhibisha na kupa mgongo.
- 17
وَسَيُجَنَّبُهَا ٱلْأَتْقَى
Unukuzi: Wa sa yujannnabuhal atqaa
Na mchamngu ataepushwa nao,
- 18
ٱلَّذِى يُؤْتِى مَالَهُۥ يَتَزَكَّىٰ
Unukuzi: Allazee yu'tee maalahoo yatazakkaa
Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa.
- 19
وَمَا لِأَحَدٍ عِندَهُۥ مِن نِّعْمَةٍۢ تُجْزَىٰٓ
Unukuzi: Wa maa li ahadin 'indahoo min ni'matin tujzaaa
Na wala si kwa kuwa yupo yeyote aliye mfanyia hisani ndio anamlipa.
- 20
إِلَّا ٱبْتِغَآءَ وَجْهِ رَبِّهِ ٱلْأَعْلَىٰ
Unukuzi: Illab tighaaa'a wajhi rabbihil a 'laa
Ila ni kutaka radhi ya Mola wake Mlezi aliye juu kabisa.
- 21
وَلَسَوْفَ يَرْضَىٰ
Unukuzi: Wa lasawfa yardaa
Naye atakuja ridhika!
Toleo la tafsiri: sw.barwani
Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).
Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.
Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.