Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia
- 1
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَٱلشَّمْسِ وَضُحَىٰهَا
Unukuzi: Wash shamsi wa duhaa haa
Naapa kwa jua na mwangaza wake!
- 2
وَٱلْقَمَرِ إِذَا تَلَىٰهَا
Unukuzi: Wal qamari izaa talaa haa
Na kwa mwezi unapo lifuatia!
- 3
وَٱلنَّهَارِ إِذَا جَلَّىٰهَا
Unukuzi: Wannahaari izaa jallaa haa
Na kwa mchana unapo lidhihirisha!
- 4
وَٱلَّيْلِ إِذَا يَغْشَىٰهَا
Unukuzi: Wallaili izaa yaghshaa haa
Na kwa usiku unapo lifunika!
- 5
وَٱلسَّمَآءِ وَمَا بَنَىٰهَا
Unukuzi: Wassamaaa'i wa maa banaahaa
Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga!
- 6
وَٱلْأَرْضِ وَمَا طَحَىٰهَا
Unukuzi: Wal ardi wa maa tahaahaa
Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza!
- 7
وَنَفْسٍۢ وَمَا سَوَّىٰهَا
Unukuzi: Wa nafsinw wa maa sawwaahaa
Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza!
- 8
فَأَلْهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقْوَىٰهَا
Unukuzi: Fa-alhamahaa fujoorahaa wa taqwaahaa
Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake,
- 9
قَدْ أَفْلَحَ مَن زَكَّىٰهَا
Unukuzi: Qad aflaha man zakkaahaa
Hakika amefanikiwa aliye itakasa,
- 10
وَقَدْ خَابَ مَن دَسَّىٰهَا
Unukuzi: Wa qad khaaba man dassaahaa
Na hakika amekhasiri aliye iviza.
- 11
كَذَّبَتْ ثَمُودُ بِطَغْوَىٰهَآ
Unukuzi: Kazzabat Samoodu bi taghwaahaaa
Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao,
- 12
إِذِ ٱنۢبَعَثَ أَشْقَىٰهَا
Unukuzi: Izim ba'asa ashqaahaa
Alipo simama mwovu wao mkubwa,
- 13
فَقَالَ لَهُمْ رَسُولُ ٱللَّهِ نَاقَةَ ٱللَّهِ وَسُقْيَٰهَا
Unukuzi: Faqaala lahum Rasoolul laahi naaqatal laahi wa suqiyaahaa
Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake.
- 14
فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمْدَمَ عَلَيْهِمْ رَبُّهُم بِذَنۢبِهِمْ فَسَوَّىٰهَا
Unukuzi: Fakazzaboohu fa'aqaroohaa fadamdama 'alaihim Rabbuhum bizambihim fasaw waahaa
Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa.
- 15
وَلَا يَخَافُ عُقْبَٰهَا
Unukuzi: Wa laa yakhaafu'uqbaahaa
Wala Yeye haogopi matokeo yake.
Toleo la tafsiri: sw.barwani
Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).
Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.
Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.