Sura zote

Surah 91

The Sun

سُورَةُ الشَّمۡسِ

Ash-Shams · Makka

Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia

Sauti
  1. 1

    بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَٱلشَّمْسِ وَضُحَىٰهَا

    Unukuzi: Wash shamsi wa duhaa haa

    Naapa kwa jua na mwangaza wake!

  2. 2

    وَٱلْقَمَرِ إِذَا تَلَىٰهَا

    Unukuzi: Wal qamari izaa talaa haa

    Na kwa mwezi unapo lifuatia!

  3. 3

    وَٱلنَّهَارِ إِذَا جَلَّىٰهَا

    Unukuzi: Wannahaari izaa jallaa haa

    Na kwa mchana unapo lidhihirisha!

  4. 4

    وَٱلَّيْلِ إِذَا يَغْشَىٰهَا

    Unukuzi: Wallaili izaa yaghshaa haa

    Na kwa usiku unapo lifunika!

  5. 5

    وَٱلسَّمَآءِ وَمَا بَنَىٰهَا

    Unukuzi: Wassamaaa'i wa maa banaahaa

    Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga!

  6. 6

    وَٱلْأَرْضِ وَمَا طَحَىٰهَا

    Unukuzi: Wal ardi wa maa tahaahaa

    Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza!

  7. 7

    وَنَفْسٍۢ وَمَا سَوَّىٰهَا

    Unukuzi: Wa nafsinw wa maa sawwaahaa

    Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza!

  8. 8

    فَأَلْهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقْوَىٰهَا

    Unukuzi: Fa-alhamahaa fujoorahaa wa taqwaahaa

    Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake,

  9. 9

    قَدْ أَفْلَحَ مَن زَكَّىٰهَا

    Unukuzi: Qad aflaha man zakkaahaa

    Hakika amefanikiwa aliye itakasa,

  10. 10

    وَقَدْ خَابَ مَن دَسَّىٰهَا

    Unukuzi: Wa qad khaaba man dassaahaa

    Na hakika amekhasiri aliye iviza.

  11. 11

    كَذَّبَتْ ثَمُودُ بِطَغْوَىٰهَآ

    Unukuzi: Kazzabat Samoodu bi taghwaahaaa

    Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao,

  12. 12

    إِذِ ٱنۢبَعَثَ أَشْقَىٰهَا

    Unukuzi: Izim ba'asa ashqaahaa

    Alipo simama mwovu wao mkubwa,

  13. 13

    فَقَالَ لَهُمْ رَسُولُ ٱللَّهِ نَاقَةَ ٱللَّهِ وَسُقْيَٰهَا

    Unukuzi: Faqaala lahum Rasoolul laahi naaqatal laahi wa suqiyaahaa

    Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake.

  14. 14

    فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمْدَمَ عَلَيْهِمْ رَبُّهُم بِذَنۢبِهِمْ فَسَوَّىٰهَا

    Unukuzi: Fakazzaboohu fa'aqaroohaa fadamdama 'alaihim Rabbuhum bizambihim fasaw waahaa

    Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa.

  15. 15

    وَلَا يَخَافُ عُقْبَٰهَا

    Unukuzi: Wa laa yakhaafu'uqbaahaa

    Wala Yeye haogopi matokeo yake.

Toleo la tafsiri: sw.barwani

Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).

Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.

Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.

The Sun — Islam Word