Sura zote

Surah 90

The City

سُورَةُ البَلَدِ

Al-Balad · Makka

Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia

Sauti
  1. 1

    بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ لَآ أُقْسِمُ بِهَٰذَا ٱلْبَلَدِ

    Unukuzi: Laaa uqsimu bihaazal balad

    Naapa kwa Mji huu!

  2. 2

    وَأَنتَ حِلٌّۢ بِهَٰذَا ٱلْبَلَدِ

    Unukuzi: Wa anta hillum bihaazal balad

    Nawe unaukaa Mji huu.

  3. 3

    وَوَالِدٍۢ وَمَا وَلَدَ

    Unukuzi: Wa waalidinw wa maa walad

    Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa.

  4. 4

    لَقَدْ خَلَقْنَا ٱلْإِنسَٰنَ فِى كَبَدٍ

    Unukuzi: Laqad khalaqnal insaana fee kabad

    Hakika tumemuumba mtu katika taabu.

  5. 5

    أَيَحْسَبُ أَن لَّن يَقْدِرَ عَلَيْهِ أَحَدٌۭ

    Unukuzi: Ayahsabu al-lai yaqdira 'alaihi ahad

    Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?

  6. 6

    يَقُولُ أَهْلَكْتُ مَالًۭا لُّبَدًا

    Unukuzi: Yaqoolu ahlaktu maalal lubadaa

    Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.

  7. 7

    أَيَحْسَبُ أَن لَّمْ يَرَهُۥٓ أَحَدٌ

    Unukuzi: Ayahsabu al lam yarahooo ahad

    Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?

  8. 8

    أَلَمْ نَجْعَل لَّهُۥ عَيْنَيْنِ

    Unukuzi: Alam naj'al lahoo 'aynayn

    Kwani hatukumpa macho mawili?

  9. 9

    وَلِسَانًۭا وَشَفَتَيْنِ

    Unukuzi: Wa lisaananw wa shafatayn

    Na ulimi, na midomo miwili?

  10. 10

    وَهَدَيْنَٰهُ ٱلنَّجْدَيْنِ

    Unukuzi: Wa hadaynaahun najdayn

    Na tukambainishia zote njia mbili?

  11. 11

    فَلَا ٱقْتَحَمَ ٱلْعَقَبَةَ

    Unukuzi: Falaq tahamal-'aqabah

    Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.

  12. 12

    وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلْعَقَبَةُ

    Unukuzi: Wa maaa adraaka mal'aqabah

    Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?

  13. 13

    فَكُّ رَقَبَةٍ

    Unukuzi: Fakku raqabah

    Kumkomboa mtumwa;

  14. 14

    أَوْ إِطْعَٰمٌۭ فِى يَوْمٍۢ ذِى مَسْغَبَةٍۢ

    Unukuzi: Aw it'aamun fee yawmin zee masghabah

    Au kumlisha siku ya njaa

  15. 15

    يَتِيمًۭا ذَا مَقْرَبَةٍ

    Unukuzi: Yateeman zaa maqrabah

    Yatima aliye jamaa,

  16. 16

    أَوْ مِسْكِينًۭا ذَا مَتْرَبَةٍۢ

    Unukuzi: Aw miskeenan zaa matrabah

    Au masikini aliye vumbini.

  17. 17

    ثُمَّ كَانَ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَتَوَاصَوْا۟ بِٱلصَّبْرِ وَتَوَاصَوْا۟ بِٱلْمَرْحَمَةِ

    Unukuzi: Summa kaana minal lazeena aamanoo wa tawaasaw bissabri wa tawaasaw bilmarhamah

    Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.

  18. 18

    أُو۟لَٰٓئِكَ أَصْحَٰبُ ٱلْمَيْمَنَةِ

    Unukuzi: Ulaaa'ika As-haabul maimanah

    Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.

  19. 19

    وَٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ بِـَٔايَٰتِنَا هُمْ أَصْحَٰبُ ٱلْمَشْـَٔمَةِ

    Unukuzi: Wallazeena kafaroo bi aayaatinaa hum as-haabul Mash'amah

    Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.

  20. 20

    عَلَيْهِمْ نَارٌۭ مُّؤْصَدَةٌۢ

    Unukuzi: Alaihim naarum mu'sadah

    Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.

Toleo la tafsiri: sw.barwani

Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).

Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.

Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.

The City — Islam Word