Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia
- 1
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَٱلْفَجْرِ
Unukuzi: Wal-Fajr
Naapa kwa alfajiri,
- 2
وَلَيَالٍ عَشْرٍۢ
Unukuzi: Wa layaalin 'ashr
Na kwa masiku kumi,
- 3
وَٱلشَّفْعِ وَٱلْوَتْرِ
Unukuzi: Wash shaf'i wal watr
Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,
- 4
وَٱلَّيْلِ إِذَا يَسْرِ
Unukuzi: Wallaili izaa yasr
Na kwa usiku unapo pita,
- 5
هَلْ فِى ذَٰلِكَ قَسَمٌۭ لِّذِى حِجْرٍ
Unukuzi: Hal fee zaalika qasamul lizee hijr
Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?
- 6
أَلَمْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ
Unukuzi: Alam tara kaifa fa'ala rabbuka bi'aad
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di?
- 7
إِرَمَ ذَاتِ ٱلْعِمَادِ
Unukuzi: Iramaa zaatil 'imaad
Wa Iram, wenye majumba marefu?
- 8
ٱلَّتِى لَمْ يُخْلَقْ مِثْلُهَا فِى ٱلْبِلَٰدِ
Unukuzi: Allatee lam yukhlaq misluhaa fil bilaad
Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?
- 9
وَثَمُودَ ٱلَّذِينَ جَابُوا۟ ٱلصَّخْرَ بِٱلْوَادِ
Unukuzi: Wa samoodal lazeena jaabus sakhra bil waad
Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?
- 10
وَفِرْعَوْنَ ذِى ٱلْأَوْتَادِ
Unukuzi: Wa fir'awna zil awtaad
Na Firauni mwenye vigingi?
- 11
ٱلَّذِينَ طَغَوْا۟ فِى ٱلْبِلَٰدِ
Unukuzi: Allazeena taghaw fil bilaad
Ambao walifanya jeuri katika nchi?
- 12
فَأَكْثَرُوا۟ فِيهَا ٱلْفَسَادَ
Unukuzi: Fa aksaroo feehal fasaad
Wakakithirisha humo ufisadi?
- 13
فَصَبَّ عَلَيْهِمْ رَبُّكَ سَوْطَ عَذَابٍ
Unukuzi: Fasabba 'alaihim Rabbuka sawta 'azaab
Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.
- 14
إِنَّ رَبَّكَ لَبِٱلْمِرْصَادِ
Unukuzi: Inna Rabbaka labil mirsaad
Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.
- 15
فَأَمَّا ٱلْإِنسَٰنُ إِذَا مَا ٱبْتَلَىٰهُ رَبُّهُۥ فَأَكْرَمَهُۥ وَنَعَّمَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّىٓ أَكْرَمَنِ
Unukuzi: Fa ammal insaanu izaa mab talaahu Rabbuhoo fa akramahoo wa na' 'amahoo fa yaqoolu Rabbeee akraman
Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!
- 16
وَأَمَّآ إِذَا مَا ٱبْتَلَىٰهُ فَقَدَرَ عَلَيْهِ رِزْقَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّىٓ أَهَٰنَنِ
Unukuzi: Wa ammaaa izaa mabtalaahu faqadara 'alaihi rizqahoo fa yaqoolu Rabbeee ahaanan
Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!
- 17
كَلَّا ۖ بَل لَّا تُكْرِمُونَ ٱلْيَتِيمَ
Unukuzi: Kalla bal laa tukrimooo nal yateem
Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,
- 18
وَلَا تَحَٰٓضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلْمِسْكِينِ
Unukuzi: Wa laa tahaaaddoona 'alaata'aamil miskeen
Wala hamhimizani kulisha masikini;
- 19
وَتَأْكُلُونَ ٱلتُّرَاثَ أَكْلًۭا لَّمًّۭا
Unukuzi: Wa taakuloonat turaasa aklal lammaa
Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,
- 20
وَتُحِبُّونَ ٱلْمَالَ حُبًّۭا جَمًّۭا
Unukuzi: Wa tuhibboonal maala hubban jammaa
Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.
- 21
كَلَّآ إِذَا دُكَّتِ ٱلْأَرْضُ دَكًّۭا دَكًّۭا
Unukuzi: Kallaaa izaaa dukkatil ardu dakkan dakka
Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,
- 22
وَجَآءَ رَبُّكَ وَٱلْمَلَكُ صَفًّۭا صَفًّۭا
Unukuzi: Wa jaaa'a Rabbuka wal malaku saffan saffaa
Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,
- 23
وَجِا۟ىٓءَ يَوْمَئِذٍۭ بِجَهَنَّمَ ۚ يَوْمَئِذٍۢ يَتَذَكَّرُ ٱلْإِنسَٰنُ وَأَنَّىٰ لَهُ ٱلذِّكْرَىٰ
Unukuzi: Wa jeee'a yawma'izim bi jahannnam; Yawma 'iziny yatazakkarul insaanu wa annaa lahuz zikraa
Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?
- 24
يَقُولُ يَٰلَيْتَنِى قَدَّمْتُ لِحَيَاتِى
Unukuzi: Yaqoolu yaa laitanee qaddamtu lihayaatee
Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!
- 25
فَيَوْمَئِذٍۢ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُۥٓ أَحَدٌۭ
Unukuzi: Fa Yawma izil laa yu'azzibu 'azaabahooo ahad
Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.
- 26
وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُۥٓ أَحَدٌۭ
Unukuzi: Wa laa yoosiqu wasaaqa hooo ahad
Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.
- 27
يَٰٓأَيَّتُهَا ٱلنَّفْسُ ٱلْمُطْمَئِنَّةُ
Unukuzi: Yaaa ayyatuhan nafsul mutma 'innah
Ewe nafsi iliyo tua!
- 28
ٱرْجِعِىٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةًۭ مَّرْضِيَّةًۭ
Unukuzi: Irji'eee ilaa Rabbiki raadiyatam mardiyyah
Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.
- 29
فَٱدْخُلِى فِى عِبَٰدِى
Unukuzi: Fadkhulee fee 'ibaadee
Basi ingia miongoni mwa waja wangu,
- 30
وَٱدْخُلِى جَنَّتِى
Unukuzi: Wadkhulee jannatee
Na ingia katika Pepo yangu.
Toleo la tafsiri: sw.barwani
Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).
Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.
Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.