Sura zote

Surah 89

The Dawn

سُورَةُ الفَجۡرِ

Al-Fajr · Makka

Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia

Sauti
  1. 1

    بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَٱلْفَجْرِ

    Unukuzi: Wal-Fajr

    Naapa kwa alfajiri,

  2. 2

    وَلَيَالٍ عَشْرٍۢ

    Unukuzi: Wa layaalin 'ashr

    Na kwa masiku kumi,

  3. 3

    وَٱلشَّفْعِ وَٱلْوَتْرِ

    Unukuzi: Wash shaf'i wal watr

    Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,

  4. 4

    وَٱلَّيْلِ إِذَا يَسْرِ

    Unukuzi: Wallaili izaa yasr

    Na kwa usiku unapo pita,

  5. 5

    هَلْ فِى ذَٰلِكَ قَسَمٌۭ لِّذِى حِجْرٍ

    Unukuzi: Hal fee zaalika qasamul lizee hijr

    Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?

  6. 6

    أَلَمْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ

    Unukuzi: Alam tara kaifa fa'ala rabbuka bi'aad

    Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di?

  7. 7

    إِرَمَ ذَاتِ ٱلْعِمَادِ

    Unukuzi: Iramaa zaatil 'imaad

    Wa Iram, wenye majumba marefu?

  8. 8

    ٱلَّتِى لَمْ يُخْلَقْ مِثْلُهَا فِى ٱلْبِلَٰدِ

    Unukuzi: Allatee lam yukhlaq misluhaa fil bilaad

    Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?

  9. 9

    وَثَمُودَ ٱلَّذِينَ جَابُوا۟ ٱلصَّخْرَ بِٱلْوَادِ

    Unukuzi: Wa samoodal lazeena jaabus sakhra bil waad

    Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?

  10. 10

    وَفِرْعَوْنَ ذِى ٱلْأَوْتَادِ

    Unukuzi: Wa fir'awna zil awtaad

    Na Firauni mwenye vigingi?

  11. 11

    ٱلَّذِينَ طَغَوْا۟ فِى ٱلْبِلَٰدِ

    Unukuzi: Allazeena taghaw fil bilaad

    Ambao walifanya jeuri katika nchi?

  12. 12

    فَأَكْثَرُوا۟ فِيهَا ٱلْفَسَادَ

    Unukuzi: Fa aksaroo feehal fasaad

    Wakakithirisha humo ufisadi?

  13. 13

    فَصَبَّ عَلَيْهِمْ رَبُّكَ سَوْطَ عَذَابٍ

    Unukuzi: Fasabba 'alaihim Rabbuka sawta 'azaab

    Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.

  14. 14

    إِنَّ رَبَّكَ لَبِٱلْمِرْصَادِ

    Unukuzi: Inna Rabbaka labil mirsaad

    Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.

  15. 15

    فَأَمَّا ٱلْإِنسَٰنُ إِذَا مَا ٱبْتَلَىٰهُ رَبُّهُۥ فَأَكْرَمَهُۥ وَنَعَّمَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّىٓ أَكْرَمَنِ

    Unukuzi: Fa ammal insaanu izaa mab talaahu Rabbuhoo fa akramahoo wa na' 'amahoo fa yaqoolu Rabbeee akraman

    Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!

  16. 16

    وَأَمَّآ إِذَا مَا ٱبْتَلَىٰهُ فَقَدَرَ عَلَيْهِ رِزْقَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّىٓ أَهَٰنَنِ

    Unukuzi: Wa ammaaa izaa mabtalaahu faqadara 'alaihi rizqahoo fa yaqoolu Rabbeee ahaanan

    Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!

  17. 17

    كَلَّا ۖ بَل لَّا تُكْرِمُونَ ٱلْيَتِيمَ

    Unukuzi: Kalla bal laa tukrimooo nal yateem

    Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,

  18. 18

    وَلَا تَحَٰٓضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلْمِسْكِينِ

    Unukuzi: Wa laa tahaaaddoona 'alaata'aamil miskeen

    Wala hamhimizani kulisha masikini;

  19. 19

    وَتَأْكُلُونَ ٱلتُّرَاثَ أَكْلًۭا لَّمًّۭا

    Unukuzi: Wa taakuloonat turaasa aklal lammaa

    Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,

  20. 20

    وَتُحِبُّونَ ٱلْمَالَ حُبًّۭا جَمًّۭا

    Unukuzi: Wa tuhibboonal maala hubban jammaa

    Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.

  21. 21

    كَلَّآ إِذَا دُكَّتِ ٱلْأَرْضُ دَكًّۭا دَكًّۭا

    Unukuzi: Kallaaa izaaa dukkatil ardu dakkan dakka

    Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,

  22. 22

    وَجَآءَ رَبُّكَ وَٱلْمَلَكُ صَفًّۭا صَفًّۭا

    Unukuzi: Wa jaaa'a Rabbuka wal malaku saffan saffaa

    Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,

  23. 23

    وَجِا۟ىٓءَ يَوْمَئِذٍۭ بِجَهَنَّمَ ۚ يَوْمَئِذٍۢ يَتَذَكَّرُ ٱلْإِنسَٰنُ وَأَنَّىٰ لَهُ ٱلذِّكْرَىٰ

    Unukuzi: Wa jeee'a yawma'izim bi jahannnam; Yawma 'iziny yatazakkarul insaanu wa annaa lahuz zikraa

    Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?

  24. 24

    يَقُولُ يَٰلَيْتَنِى قَدَّمْتُ لِحَيَاتِى

    Unukuzi: Yaqoolu yaa laitanee qaddamtu lihayaatee

    Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!

  25. 25

    فَيَوْمَئِذٍۢ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُۥٓ أَحَدٌۭ

    Unukuzi: Fa Yawma izil laa yu'azzibu 'azaabahooo ahad

    Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.

  26. 26

    وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُۥٓ أَحَدٌۭ

    Unukuzi: Wa laa yoosiqu wasaaqa hooo ahad

    Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.

  27. 27

    يَٰٓأَيَّتُهَا ٱلنَّفْسُ ٱلْمُطْمَئِنَّةُ

    Unukuzi: Yaaa ayyatuhan nafsul mutma 'innah

    Ewe nafsi iliyo tua!

  28. 28

    ٱرْجِعِىٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةًۭ مَّرْضِيَّةًۭ

    Unukuzi: Irji'eee ilaa Rabbiki raadiyatam mardiyyah

    Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.

  29. 29

    فَٱدْخُلِى فِى عِبَٰدِى

    Unukuzi: Fadkhulee fee 'ibaadee

    Basi ingia miongoni mwa waja wangu,

  30. 30

    وَٱدْخُلِى جَنَّتِى

    Unukuzi: Wadkhulee jannatee

    Na ingia katika Pepo yangu.

Toleo la tafsiri: sw.barwani

Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).

Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.

Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.

The Dawn — Islam Word