Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia
- 1
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلْغَٰشِيَةِ
Unukuzi: Hal ataaka hadeesul ghaashiyah
Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?
- 2
وُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍ خَٰشِعَةٌ
Unukuzi: Wujoohuny yawma 'izin khaashi'ah
Siku hiyo nyuso zitainama,
- 3
عَامِلَةٌۭ نَّاصِبَةٌۭ
Unukuzi: 'Aamilatun naasibah
Zikifanya kazi, nazo taabani.
- 4
تَصْلَىٰ نَارًا حَامِيَةًۭ
Unukuzi: Taslaa naaran haamiyah
Ziingie katika Moto unao waka -
- 5
تُسْقَىٰ مِنْ عَيْنٍ ءَانِيَةٍۢ
Unukuzi: Tusqaa min 'aynin aaniyah
Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.
- 6
لَّيْسَ لَهُمْ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٍۢ
Unukuzi: Laisa lahum ta'aamun illaa min daree'
Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.
- 7
لَّا يُسْمِنُ وَلَا يُغْنِى مِن جُوعٍۢ
Unukuzi: Laa yusminu wa laa yughnee min joo'
Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.
- 8
وُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍۢ نَّاعِمَةٌۭ
Unukuzi: Wujoohuny yawma 'izin naa'imah
Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.
- 9
لِّسَعْيِهَا رَاضِيَةٌۭ
Unukuzi: Lisa'yihaa raadiyah
Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,
- 10
فِى جَنَّةٍ عَالِيَةٍۢ
Unukuzi: Fee jannatin 'aaliyah
Katika Bustani ya juu.
- 11
لَّا تَسْمَعُ فِيهَا لَٰغِيَةًۭ
Unukuzi: Laa tasma'u feehaa laaghiyah
Hawatasikia humo upuuzi.
- 12
فِيهَا عَيْنٌۭ جَارِيَةٌۭ
Unukuzi: Feehaa 'aynun jaariyah
Humo imo chemchem inayo miminika.
- 13
فِيهَا سُرُرٌۭ مَّرْفُوعَةٌۭ
Unukuzi: Feehaa sururum marfoo'ah
Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,
- 14
وَأَكْوَابٌۭ مَّوْضُوعَةٌۭ
Unukuzi: Wa akwaabum mawdoo 'ah
Na bilauri zilizo pangwa,
- 15
وَنَمَارِقُ مَصْفُوفَةٌۭ
Unukuzi: Wa namaariqu masfoofah
Na matakia safu safu,
- 16
وَزَرَابِىُّ مَبْثُوثَةٌ
Unukuzi: Wa zaraabiyyu mabsoosah
Na mazulia yaliyo tandikwa.
- 17
أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى ٱلْإِبِلِ كَيْفَ خُلِقَتْ
Unukuzi: Afalaa yanzuroona ilalibili kaifa khuliqat
Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?
- 18
وَإِلَى ٱلسَّمَآءِ كَيْفَ رُفِعَتْ
Unukuzi: Wa ilas samaaa'i kaifa rufi'at
Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?
- 19
وَإِلَى ٱلْجِبَالِ كَيْفَ نُصِبَتْ
Unukuzi: Wa ilal jibaali kaifa nusibat
Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?
- 20
وَإِلَى ٱلْأَرْضِ كَيْفَ سُطِحَتْ
Unukuzi: Wa ilal ardi kaifa sutihat
Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?
- 21
فَذَكِّرْ إِنَّمَآ أَنتَ مُذَكِّرٌۭ
Unukuzi: Fazakkir innama anta Muzakkir
Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.
- 22
لَّسْتَ عَلَيْهِم بِمُصَيْطِرٍ
Unukuzi: Lasta 'alaihim bimusaitir
Wewe si mwenye kuwatawalia.
- 23
إِلَّا مَن تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ
Unukuzi: Illaa man tawallaa wa kafar
Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,
- 24
فَيُعَذِّبُهُ ٱللَّهُ ٱلْعَذَابَ ٱلْأَكْبَرَ
Unukuzi: Fa yu'azzibuhul laahul 'azaabal akbar
Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!
- 25
إِنَّ إِلَيْنَآ إِيَابَهُمْ
Unukuzi: Innaa ilainaaa iyaabahum
Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.
- 26
ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا حِسَابَهُم
Unukuzi: Summa inna 'alainaa hisaabahum
Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!
Toleo la tafsiri: sw.barwani
Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).
Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.
Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.