Sura zote

Surah 88

The Overwhelming

سُورَةُ الغَاشِيَةِ

Al-Ghaashiya · Makka

Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia

Sauti
  1. 1

    بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلْغَٰشِيَةِ

    Unukuzi: Hal ataaka hadeesul ghaashiyah

    Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?

  2. 2

    وُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍ خَٰشِعَةٌ

    Unukuzi: Wujoohuny yawma 'izin khaashi'ah

    Siku hiyo nyuso zitainama,

  3. 3

    عَامِلَةٌۭ نَّاصِبَةٌۭ

    Unukuzi: 'Aamilatun naasibah

    Zikifanya kazi, nazo taabani.

  4. 4

    تَصْلَىٰ نَارًا حَامِيَةًۭ

    Unukuzi: Taslaa naaran haamiyah

    Ziingie katika Moto unao waka -

  5. 5

    تُسْقَىٰ مِنْ عَيْنٍ ءَانِيَةٍۢ

    Unukuzi: Tusqaa min 'aynin aaniyah

    Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.

  6. 6

    لَّيْسَ لَهُمْ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٍۢ

    Unukuzi: Laisa lahum ta'aamun illaa min daree'

    Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.

  7. 7

    لَّا يُسْمِنُ وَلَا يُغْنِى مِن جُوعٍۢ

    Unukuzi: Laa yusminu wa laa yughnee min joo'

    Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.

  8. 8

    وُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍۢ نَّاعِمَةٌۭ

    Unukuzi: Wujoohuny yawma 'izin naa'imah

    Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.

  9. 9

    لِّسَعْيِهَا رَاضِيَةٌۭ

    Unukuzi: Lisa'yihaa raadiyah

    Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,

  10. 10

    فِى جَنَّةٍ عَالِيَةٍۢ

    Unukuzi: Fee jannatin 'aaliyah

    Katika Bustani ya juu.

  11. 11

    لَّا تَسْمَعُ فِيهَا لَٰغِيَةًۭ

    Unukuzi: Laa tasma'u feehaa laaghiyah

    Hawatasikia humo upuuzi.

  12. 12

    فِيهَا عَيْنٌۭ جَارِيَةٌۭ

    Unukuzi: Feehaa 'aynun jaariyah

    Humo imo chemchem inayo miminika.

  13. 13

    فِيهَا سُرُرٌۭ مَّرْفُوعَةٌۭ

    Unukuzi: Feehaa sururum marfoo'ah

    Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,

  14. 14

    وَأَكْوَابٌۭ مَّوْضُوعَةٌۭ

    Unukuzi: Wa akwaabum mawdoo 'ah

    Na bilauri zilizo pangwa,

  15. 15

    وَنَمَارِقُ مَصْفُوفَةٌۭ

    Unukuzi: Wa namaariqu masfoofah

    Na matakia safu safu,

  16. 16

    وَزَرَابِىُّ مَبْثُوثَةٌ

    Unukuzi: Wa zaraabiyyu mabsoosah

    Na mazulia yaliyo tandikwa.

  17. 17

    أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى ٱلْإِبِلِ كَيْفَ خُلِقَتْ

    Unukuzi: Afalaa yanzuroona ilalibili kaifa khuliqat

    Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?

  18. 18

    وَإِلَى ٱلسَّمَآءِ كَيْفَ رُفِعَتْ

    Unukuzi: Wa ilas samaaa'i kaifa rufi'at

    Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?

  19. 19

    وَإِلَى ٱلْجِبَالِ كَيْفَ نُصِبَتْ

    Unukuzi: Wa ilal jibaali kaifa nusibat

    Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?

  20. 20

    وَإِلَى ٱلْأَرْضِ كَيْفَ سُطِحَتْ

    Unukuzi: Wa ilal ardi kaifa sutihat

    Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?

  21. 21

    فَذَكِّرْ إِنَّمَآ أَنتَ مُذَكِّرٌۭ

    Unukuzi: Fazakkir innama anta Muzakkir

    Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.

  22. 22

    لَّسْتَ عَلَيْهِم بِمُصَيْطِرٍ

    Unukuzi: Lasta 'alaihim bimusaitir

    Wewe si mwenye kuwatawalia.

  23. 23

    إِلَّا مَن تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ

    Unukuzi: Illaa man tawallaa wa kafar

    Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,

  24. 24

    فَيُعَذِّبُهُ ٱللَّهُ ٱلْعَذَابَ ٱلْأَكْبَرَ

    Unukuzi: Fa yu'azzibuhul laahul 'azaabal akbar

    Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!

  25. 25

    إِنَّ إِلَيْنَآ إِيَابَهُمْ

    Unukuzi: Innaa ilainaaa iyaabahum

    Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.

  26. 26

    ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا حِسَابَهُم

    Unukuzi: Summa inna 'alainaa hisaabahum

    Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!

Toleo la tafsiri: sw.barwani

Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).

Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.

Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.