Sura zote

Surah 87

The Most High

سُورَةُ الأَعۡلَىٰ

Al-A'laa · Makka

Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia

Sauti
  1. 1

    بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ سَبِّحِ ٱسْمَ رَبِّكَ ٱلْأَعْلَى

    Unukuzi: Sabbihisma Rabbikal A'laa

    Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa,

  2. 2

    ٱلَّذِى خَلَقَ فَسَوَّىٰ

    Unukuzi: Allazee khalaqa fasawwaa

    Aliye umba, na akaweka sawa,

  3. 3

    وَٱلَّذِى قَدَّرَ فَهَدَىٰ

    Unukuzi: Wallazee qaddara fahadaa

    Na ambaye amekadiria na akaongoa,

  4. 4

    وَٱلَّذِىٓ أَخْرَجَ ٱلْمَرْعَىٰ

    Unukuzi: Wallazeee akhrajal mar'aa

    Na aliye otesha malisho,

  5. 5

    فَجَعَلَهُۥ غُثَآءً أَحْوَىٰ

    Unukuzi: Faja'alahoo ghusaaa'an ahwaa

    Kisha akayafanya makavu, meusi.

  6. 6

    سَنُقْرِئُكَ فَلَا تَنسَىٰٓ

    Unukuzi: Sanuqri'uka falaa tansaaa

    Tutakusomesha wala hutasahau,

  7. 7

    إِلَّا مَا شَآءَ ٱللَّهُ ۚ إِنَّهُۥ يَعْلَمُ ٱلْجَهْرَ وَمَا يَخْفَىٰ

    Unukuzi: Illaa maa shaaa'al laah; innahoo ya'lamul jahra wa maa yakhfaa

    Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana.

  8. 8

    وَنُيَسِّرُكَ لِلْيُسْرَىٰ

    Unukuzi: Wa nu-yassiruka lilyusraa

    Na tutakusahilishia yawe mepesi.

  9. 9

    فَذَكِّرْ إِن نَّفَعَتِ ٱلذِّكْرَىٰ

    Unukuzi: Fazakkir in nafa'atizzikraa

    Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa.

  10. 10

    سَيَذَّكَّرُ مَن يَخْشَىٰ

    Unukuzi: Sa yazzakkaru maiyakhshaa

    Atakumbuka mwenye kuogopa.

  11. 11

    وَيَتَجَنَّبُهَا ٱلْأَشْقَى

    Unukuzi: Wa yatajannabuhal ashqaa

    Na atajitenga mbali nayo mpotovu,

  12. 12

    ٱلَّذِى يَصْلَى ٱلنَّارَ ٱلْكُبْرَىٰ

    Unukuzi: Allazee yaslan Naaral kubraa

    Ambaye atauingia Moto mkubwa.

  13. 13

    ثُمَّ لَا يَمُوتُ فِيهَا وَلَا يَحْيَىٰ

    Unukuzi: Summa laa yamootu feehaa wa laa yahyaa

    Tena humo hatakufa wala hawi hai.

  14. 14

    قَدْ أَفْلَحَ مَن تَزَكَّىٰ

    Unukuzi: Qad aflaha man tazakkaa

    Hakika amekwisha fanikiwa aliye jitakasa.

  15. 15

    وَذَكَرَ ٱسْمَ رَبِّهِۦ فَصَلَّىٰ

    Unukuzi: Wa zakaras ma Rabbihee fasallaa

    Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akasali.

  16. 16

    بَلْ تُؤْثِرُونَ ٱلْحَيَوٰةَ ٱلدُّنْيَا

    Unukuzi: Bal tu'siroonal hayaatad dunyaa

    Lakini nyinyi mnakhiari maisha ya dunia!

  17. 17

    وَٱلْءَاخِرَةُ خَيْرٌۭ وَأَبْقَىٰٓ

    Unukuzi: Wal Aakhiratu khairunw wa abqaa

    Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi.

  18. 18

    إِنَّ هَٰذَا لَفِى ٱلصُّحُفِ ٱلْأُولَىٰ

    Unukuzi: Inna haazaa lafis suhu fil oolaa

    Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,

  19. 19

    صُحُفِ إِبْرَٰهِيمَ وَمُوسَىٰ

    Unukuzi: Suhufi Ibraaheema wa Moosaa

    Vitabu vya Ibrahimu na Musa.

Toleo la tafsiri: sw.barwani

Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).

Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.

Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.

The Most High — Islam Word