Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia
- 1
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ سَبِّحِ ٱسْمَ رَبِّكَ ٱلْأَعْلَى
Unukuzi: Sabbihisma Rabbikal A'laa
Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa,
- 2
ٱلَّذِى خَلَقَ فَسَوَّىٰ
Unukuzi: Allazee khalaqa fasawwaa
Aliye umba, na akaweka sawa,
- 3
وَٱلَّذِى قَدَّرَ فَهَدَىٰ
Unukuzi: Wallazee qaddara fahadaa
Na ambaye amekadiria na akaongoa,
- 4
وَٱلَّذِىٓ أَخْرَجَ ٱلْمَرْعَىٰ
Unukuzi: Wallazeee akhrajal mar'aa
Na aliye otesha malisho,
- 5
فَجَعَلَهُۥ غُثَآءً أَحْوَىٰ
Unukuzi: Faja'alahoo ghusaaa'an ahwaa
Kisha akayafanya makavu, meusi.
- 6
سَنُقْرِئُكَ فَلَا تَنسَىٰٓ
Unukuzi: Sanuqri'uka falaa tansaaa
Tutakusomesha wala hutasahau,
- 7
إِلَّا مَا شَآءَ ٱللَّهُ ۚ إِنَّهُۥ يَعْلَمُ ٱلْجَهْرَ وَمَا يَخْفَىٰ
Unukuzi: Illaa maa shaaa'al laah; innahoo ya'lamul jahra wa maa yakhfaa
Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana.
- 8
وَنُيَسِّرُكَ لِلْيُسْرَىٰ
Unukuzi: Wa nu-yassiruka lilyusraa
Na tutakusahilishia yawe mepesi.
- 9
فَذَكِّرْ إِن نَّفَعَتِ ٱلذِّكْرَىٰ
Unukuzi: Fazakkir in nafa'atizzikraa
Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa.
- 10
سَيَذَّكَّرُ مَن يَخْشَىٰ
Unukuzi: Sa yazzakkaru maiyakhshaa
Atakumbuka mwenye kuogopa.
- 11
وَيَتَجَنَّبُهَا ٱلْأَشْقَى
Unukuzi: Wa yatajannabuhal ashqaa
Na atajitenga mbali nayo mpotovu,
- 12
ٱلَّذِى يَصْلَى ٱلنَّارَ ٱلْكُبْرَىٰ
Unukuzi: Allazee yaslan Naaral kubraa
Ambaye atauingia Moto mkubwa.
- 13
ثُمَّ لَا يَمُوتُ فِيهَا وَلَا يَحْيَىٰ
Unukuzi: Summa laa yamootu feehaa wa laa yahyaa
Tena humo hatakufa wala hawi hai.
- 14
قَدْ أَفْلَحَ مَن تَزَكَّىٰ
Unukuzi: Qad aflaha man tazakkaa
Hakika amekwisha fanikiwa aliye jitakasa.
- 15
وَذَكَرَ ٱسْمَ رَبِّهِۦ فَصَلَّىٰ
Unukuzi: Wa zakaras ma Rabbihee fasallaa
Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akasali.
- 16
بَلْ تُؤْثِرُونَ ٱلْحَيَوٰةَ ٱلدُّنْيَا
Unukuzi: Bal tu'siroonal hayaatad dunyaa
Lakini nyinyi mnakhiari maisha ya dunia!
- 17
وَٱلْءَاخِرَةُ خَيْرٌۭ وَأَبْقَىٰٓ
Unukuzi: Wal Aakhiratu khairunw wa abqaa
Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi.
- 18
إِنَّ هَٰذَا لَفِى ٱلصُّحُفِ ٱلْأُولَىٰ
Unukuzi: Inna haazaa lafis suhu fil oolaa
Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,
- 19
صُحُفِ إِبْرَٰهِيمَ وَمُوسَىٰ
Unukuzi: Suhufi Ibraaheema wa Moosaa
Vitabu vya Ibrahimu na Musa.
Toleo la tafsiri: sw.barwani
Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).
Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.
Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.