Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia
- 1
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَٱلسَّمَآءِ وَٱلطَّارِقِ
Unukuzi: Wassamaaa'i wattaariq
Naapa kwa mbingu na Kinacho kuja usiku!
- 2
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلطَّارِقُ
Unukuzi: Wa maaa adraaka mattaariq
Na nini kitakacho kujuulisha ni nini hicho Kinacho kuja usiku?
- 3
ٱلنَّجْمُ ٱلثَّاقِبُ
Unukuzi: Annajmus saaqib
Ni Nyota yenye mwanga mkali.
- 4
إِن كُلُّ نَفْسٍۢ لَّمَّا عَلَيْهَا حَافِظٌۭ
Unukuzi: In kullu nafsil lammaa 'alaihaa haafiz
Hapana nafsi ila inayo mwangalizi.
- 5
فَلْيَنظُرِ ٱلْإِنسَٰنُ مِمَّ خُلِقَ
Unukuzi: Fal yanzuril insaanu mimma khuliq
Hebu naajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani?
- 6
خُلِقَ مِن مَّآءٍۢ دَافِقٍۢ
Unukuzi: Khuliqa mim maaa'in daafiq
Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa,
- 7
يَخْرُجُ مِنۢ بَيْنِ ٱلصُّلْبِ وَٱلتَّرَآئِبِ
Unukuzi: Yakhruju mim bainissulbi wat taraaa'ib
Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu.
- 8
إِنَّهُۥ عَلَىٰ رَجْعِهِۦ لَقَادِرٌۭ
Unukuzi: Innahoo 'alaa raj'ihee laqaadir
Hakika Yeye ana uweza wa kumrudisha.
- 9
يَوْمَ تُبْلَى ٱلسَّرَآئِرُ
Unukuzi: Yawma tublas saraaa'ir
Siku zitakapo dhihirishwa siri.
- 10
فَمَا لَهُۥ مِن قُوَّةٍۢ وَلَا نَاصِرٍۢ
Unukuzi: Famaa lahoo min quwwatinw wa laa naasir
Basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi.
- 11
وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلرَّجْعِ
Unukuzi: Wassamaaa'i zaatir raj'
Naapa kwa mbingu yenye marejeo!
- 12
وَٱلْأَرْضِ ذَاتِ ٱلصَّدْعِ
Unukuzi: Wal ardi zaatis sad'
Na kwa ardhi inayo pasuka!
- 13
إِنَّهُۥ لَقَوْلٌۭ فَصْلٌۭ
Unukuzi: Innahoo laqawlun fasl
Hakika hii ni kauli ya kupambanua.
- 14
وَمَا هُوَ بِٱلْهَزْلِ
Unukuzi: Wa maa huwa bil hazl
Wala si mzaha.
- 15
إِنَّهُمْ يَكِيدُونَ كَيْدًۭا
Unukuzi: Innahum yakeedoona kaidaa
Hakika wao wanapanga mpango.
- 16
وَأَكِيدُ كَيْدًۭا
Unukuzi: Wa akeedu kaidaa
Na Mimi napanga mpango.
- 17
فَمَهِّلِ ٱلْكَٰفِرِينَ أَمْهِلْهُمْ رُوَيْدًۢا
Unukuzi: Famahhilil kaafireena amhilhum ruwaidaa
Basi wape muhula makafiri - wape muhula pole pole.
Toleo la tafsiri: sw.barwani
Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).
Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.
Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.