Sura zote

Surah 85

The Mansions of the Stars

سُورَةُ البُرُوجِ

Al-Burooj · Makka

Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia

Sauti
  1. 1

    بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلْبُرُوجِ

    Unukuzi: Wassamaaa'i zaatil burooj

    Naapa kwa mbingu yenye Buruji!

  2. 2

    وَٱلْيَوْمِ ٱلْمَوْعُودِ

    Unukuzi: Wal yawmil maw'ood

    Na kwa siku iliyo ahidiwa!

  3. 3

    وَشَاهِدٍۢ وَمَشْهُودٍۢ

    Unukuzi: Wa shaahidinw wa mashhood

    Na kwa shahidi na kinacho shuhudiwa!

  4. 4

    قُتِلَ أَصْحَٰبُ ٱلْأُخْدُودِ

    Unukuzi: Qutila as haabul ukhdood

    Wameangamizwa watu wa makhandaki

  5. 5

    ٱلنَّارِ ذَاتِ ٱلْوَقُودِ

    Unukuzi: Annaari zaatil waqood

    Yenye moto wenye kuni nyingi,

  6. 6

    إِذْ هُمْ عَلَيْهَا قُعُودٌۭ

    Unukuzi: Iz hum 'alaihaa qu'ood

    Walipo kuwa wamekaa hapo,

  7. 7

    وَهُمْ عَلَىٰ مَا يَفْعَلُونَ بِٱلْمُؤْمِنِينَ شُهُودٌۭ

    Unukuzi: Wa hum 'alaa maa yaf'aloona bilmu 'mineena shuhood

    Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini.

  8. 8

    وَمَا نَقَمُوا۟ مِنْهُمْ إِلَّآ أَن يُؤْمِنُوا۟ بِٱللَّهِ ٱلْعَزِيزِ ٱلْحَمِيدِ

    Unukuzi: Wa maa naqamoo minhum illaaa aiyu'minoo billaahil 'azeezil Hameed

    Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Msifiwa,

  9. 9

    ٱلَّذِى لَهُۥ مُلْكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ ۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَىْءٍۢ شَهِيدٌ

    Unukuzi: Allazee lahoo mulkus samaawaati wal ard; wallaahu 'alaa kulli shai 'in Shaheed

    Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni shaahidi wa kila kitu.

  10. 10

    إِنَّ ٱلَّذِينَ فَتَنُوا۟ ٱلْمُؤْمِنِينَ وَٱلْمُؤْمِنَٰتِ ثُمَّ لَمْ يَتُوبُوا۟ فَلَهُمْ عَذَابُ جَهَنَّمَ وَلَهُمْ عَذَابُ ٱلْحَرِيقِ

    Unukuzi: Innal lazeena fatanul mu'mineena wal mu'minaati summa lam yatooboo falahum 'azaabu Jahannama wa lahum 'azaabul hareeq

    Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua.

  11. 11

    إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَهُمْ جَنَّٰتٌۭ تَجْرِى مِن تَحْتِهَا ٱلْأَنْهَٰرُ ۚ ذَٰلِكَ ٱلْفَوْزُ ٱلْكَبِيرُ

    Unukuzi: Innal lazeena aamanoo wa 'amilus saalihaati lahum Jannaatun tajree min tahtihal anhaar; zaalikal fawzul kabeer

    Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa.

  12. 12

    إِنَّ بَطْشَ رَبِّكَ لَشَدِيدٌ

    Unukuzi: Inna batsha Rabbika lashadeed

    Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali.

  13. 13

    إِنَّهُۥ هُوَ يُبْدِئُ وَيُعِيدُ

    Unukuzi: Innahoo Huwa yubdi'u wa yu'eed

    Yeye ndiye anaye anzisha na ndiye anaye rejeza tena,

  14. 14

    وَهُوَ ٱلْغَفُورُ ٱلْوَدُودُ

    Unukuzi: Wa Huwal Ghafoorul Wadood

    Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi,

  15. 15

    ذُو ٱلْعَرْشِ ٱلْمَجِيدُ

    Unukuzi: Zul 'Arshil Majeed

    Mwenye Kiti cha Enzi, Mtukufu,

  16. 16

    فَعَّالٌۭ لِّمَا يُرِيدُ

    Unukuzi: Fa' 'aalul limaa yureed

    Atendaye ayatakayo.

  17. 17

    هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلْجُنُودِ

    Unukuzi: Hal ataaka hadeesul junood

    Je! Zimekuwasilia khabari za majeshi?

  18. 18

    فِرْعَوْنَ وَثَمُودَ

    Unukuzi: Fir'awna wa Samood

    Ya Firauni na Thamudi?

  19. 19

    بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ فِى تَكْذِيبٍۢ

    Unukuzi: Balil lazeena kafaroo fee takzeeb

    Lakini walio kufuru wamo katika kukadhibisha.

  20. 20

    وَٱللَّهُ مِن وَرَآئِهِم مُّحِيطٌۢ

    Unukuzi: Wallaahu minw waraaa'ihim muheet

    Na Mwenyezi Mungu nyuma yao amewazunguka.

  21. 21

    بَلْ هُوَ قُرْءَانٌۭ مَّجِيدٌۭ

    Unukuzi: Bal huwa Quraanum Majeed

    Bali hii ni Qur'ani tukufu

  22. 22

    فِى لَوْحٍۢ مَّحْفُوظٍۭ

    Unukuzi: Fee Lawhim Mahfooz

    Katika Ubao Ulio Hifadhiwa.

Toleo la tafsiri: sw.barwani

Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).

Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.

Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.

The Mansions of the Stars — Islam Word