Sura zote

Surah 84

The Sundering

سُورَةُ الانشِقَاقِ

Al-Inshiqaaq · Makka

Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia

Sauti
  1. 1

    بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنشَقَّتْ

    Unukuzi: Izas samaaa'un shaqqat

    Itapo chanika mbingu,

  2. 2

    وَأَذِنَتْ لِرَبِّهَا وَحُقَّتْ

    Unukuzi: Wa azinat li Rabbihaa wa huqqat

    Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,

  3. 3

    وَإِذَا ٱلْأَرْضُ مُدَّتْ

    Unukuzi: Wa izal ardu muddat

    Na ardhi itakapo tanuliwa,

  4. 4

    وَأَلْقَتْ مَا فِيهَا وَتَخَلَّتْ

    Unukuzi: Wa alqat maa feehaa wa takhallat

    Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu,

  5. 5

    وَأَذِنَتْ لِرَبِّهَا وَحُقَّتْ

    Unukuzi: Wa azinat li Rabbihaa wa huqqat

    Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,

  6. 6

    يَٰٓأَيُّهَا ٱلْإِنسَٰنُ إِنَّكَ كَادِحٌ إِلَىٰ رَبِّكَ كَدْحًۭا فَمُلَٰقِيهِ

    Unukuzi: Yaaa ayyuhal insaanu innaka kaadihun ilaa Rabbika kad han famulaaqeeh

    Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta.

  7. 7

    فَأَمَّا مَنْ أُوتِىَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ

    Unukuzi: Fa ammaa man ootiya kitaabahoo biyameenih

    Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia,

  8. 8

    فَسَوْفَ يُحَاسَبُ حِسَابًۭا يَسِيرًۭا

    Unukuzi: Fasawfa yuhaasabu hi saabai yaseeraa

    Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi,

  9. 9

    وَيَنقَلِبُ إِلَىٰٓ أَهْلِهِۦ مَسْرُورًۭا

    Unukuzi: Wa yanqalibu ilaaa ahlihee masrooraa

    Na arudi kwa ahali zake na furaha.

  10. 10

    وَأَمَّا مَنْ أُوتِىَ كِتَٰبَهُۥ وَرَآءَ ظَهْرِهِۦ

    Unukuzi: Wa ammaa man ootiya kitaabahoo waraaa'a zahrih

    Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake,

  11. 11

    فَسَوْفَ يَدْعُوا۟ ثُبُورًۭا

    Unukuzi: Fasawfa yad'oo subooraa

    Basi huyo ataomba kuteketea.

  12. 12

    وَيَصْلَىٰ سَعِيرًا

    Unukuzi: Wa yaslaa sa'eeraa

    Na ataingia Motoni.

  13. 13

    إِنَّهُۥ كَانَ فِىٓ أَهْلِهِۦ مَسْرُورًا

    Unukuzi: Innahoo kaana feee ahlihee masrooraa

    Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake.

  14. 14

    إِنَّهُۥ ظَنَّ أَن لَّن يَحُورَ

    Unukuzi: Innahoo zanna al lai yahoor

    Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena.

  15. 15

    بَلَىٰٓ إِنَّ رَبَّهُۥ كَانَ بِهِۦ بَصِيرًۭا

    Unukuzi: Balaaa inna Rabbahoo kaana bihee baseeraa

    Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona!

  16. 16

    فَلَآ أُقْسِمُ بِٱلشَّفَقِ

    Unukuzi: Falaaa uqsimu bishshafaq

    Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa,

  17. 17

    وَٱلَّيْلِ وَمَا وَسَقَ

    Unukuzi: Wallaili wa maa wasaq

    Na kwa usiku na unavyo vikusanya,

  18. 18

    وَٱلْقَمَرِ إِذَا ٱتَّسَقَ

    Unukuzi: Walqamari izat tasaq

    Na kwa mwezi unapo pevuka,

  19. 19

    لَتَرْكَبُنَّ طَبَقًا عَن طَبَقٍۢ

    Unukuzi: Latarkabunna tabaqan 'an tabaq

    Lazima mtapanda t'abaka kwa t'abaka!

  20. 20

    فَمَا لَهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ

    Unukuzi: Famaa lahum laa yu'minoon

    Basi wana nini hawaamini?

  21. 21

    وَإِذَا قُرِئَ عَلَيْهِمُ ٱلْقُرْءَانُ لَا يَسْجُدُونَ ۩

    Unukuzi: Wa izaa quri'a 'alaihimul Quraanu laa yasjudoon

    Na wanapo somewa Qur'ani hawasujudu?

  22. 22

    بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ يُكَذِّبُونَ

    Unukuzi: Balil lazeena kafaroo yukazziboon

    Bali walio kufuru wanakanusha tu.

  23. 23

    وَٱللَّهُ أَعْلَمُ بِمَا يُوعُونَ

    Unukuzi: Wallaahu a'lamu bimaa yoo'oon

    Na Mwenyezi Mungu anajua wanayo yadhamiria.

  24. 24

    فَبَشِّرْهُم بِعَذَابٍ أَلِيمٍ

    Unukuzi: Fabashshirhum bi'azaabin aleem

    Basi wabashirie adhabu chungu!

  25. 25

    إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَهُمْ أَجْرٌ غَيْرُ مَمْنُونٍۭ

    Unukuzi: Illal lazeena aamanoo wa 'amilus saalihaati lahum ajrun ghairu mamnoon

    Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usio malizika.

Toleo la tafsiri: sw.barwani

Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).

Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.

Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.

The Sundering — Islam Word