Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia
- 1
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَيْلٌۭ لِّلْمُطَفِّفِينَ
Unukuzi: Wailul lil mutaffifeen
Ole wao hao wapunjao!
- 2
ٱلَّذِينَ إِذَا ٱكْتَالُوا۟ عَلَى ٱلنَّاسِ يَسْتَوْفُونَ
Unukuzi: Allazeena izak taaloo 'alan naasi yastawfoon
Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.
- 3
وَإِذَا كَالُوهُمْ أَو وَّزَنُوهُمْ يُخْسِرُونَ
Unukuzi: Wa izaa kaaloohum aw wazanoohum yukhsiroon
Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.
- 4
أَلَا يَظُنُّ أُو۟لَٰٓئِكَ أَنَّهُم مَّبْعُوثُونَ
Unukuzi: Alaa yazunnu ulaaa'ika annahum mab'oosoon
Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa
- 5
لِيَوْمٍ عَظِيمٍۢ
Unukuzi: Li Yawmin 'Azeem
Katika Siku iliyo kuu,
- 6
يَوْمَ يَقُومُ ٱلنَّاسُ لِرَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ
Unukuzi: Yawma yaqoomun naasu li Rabbil 'aalameen
Siku watapo msimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?
- 7
كَلَّآ إِنَّ كِتَٰبَ ٱلْفُجَّارِ لَفِى سِجِّينٍۢ
Unukuzi: Kallaaa inna kitaabal fujjaari lafee Sijjeen
Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.
- 8
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا سِجِّينٌۭ
Unukuzi: Wa maa adraaka maa Sijjeen
Unajua nini Sijjin?
- 9
كِتَٰبٌۭ مَّرْقُومٌۭ
Unukuzi: Kitaabum marqoom
Kitabu kilicho andikwa.
- 10
وَيْلٌۭ يَوْمَئِذٍۢ لِّلْمُكَذِّبِينَ
Unukuzi: Wailuny yawma'izil lil mukazzibeen
Ole wao siku hiyo kwa wanao kadhibisha!
- 11
ٱلَّذِينَ يُكَذِّبُونَ بِيَوْمِ ٱلدِّينِ
Unukuzi: Allazeena yukazziboona bi yawmid deen
Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.
- 12
وَمَا يُكَذِّبُ بِهِۦٓ إِلَّا كُلُّ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ
Unukuzi: Wa maa yukazzibu biheee illaa kullu mu'tadin aseem
Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.
- 13
إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ ءَايَٰتُنَا قَالَ أَسَٰطِيرُ ٱلْأَوَّلِينَ
Unukuzi: Izaa tutlaa'alaihi aayaatunaa qaala asaateerul awwaleen
Anapo somewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale!
- 14
كَلَّا ۖ بَلْ ۜ رَانَ عَلَىٰ قُلُوبِهِم مَّا كَانُوا۟ يَكْسِبُونَ
Unukuzi: Kallaa bal raana 'alaa quloobihim maa kaanoo yaksiboon
Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao walio kuwa wakiyachuma.
- 15
كَلَّآ إِنَّهُمْ عَن رَّبِّهِمْ يَوْمَئِذٍۢ لَّمَحْجُوبُونَ
Unukuzi: Kallaaa innahum 'ar Rabbihim yawma'izil lamah jooboon
Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi.
- 16
ثُمَّ إِنَّهُمْ لَصَالُوا۟ ٱلْجَحِيمِ
Unukuzi: Summa innahum lasaa lul jaheem
Kisha wataingia Motoni!
- 17
ثُمَّ يُقَالُ هَٰذَا ٱلَّذِى كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ
Unukuzi: Summa yuqaalu haazal lazee kuntum bihee tukazziboon
Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyakadhabisha.
- 18
كَلَّآ إِنَّ كِتَٰبَ ٱلْأَبْرَارِ لَفِى عِلِّيِّينَ
Unukuzi: Kallaaa inna kitaabal abraari lafee'Illiyyeen
Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I'liyyin.
- 19
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا عِلِّيُّونَ
Unukuzi: Wa maaa adraaka maa 'Illiyyoon
Na nini kitakacho kujuvya nini I'liyyin?
- 20
كِتَٰبٌۭ مَّرْقُومٌۭ
Unukuzi: Kitaabum marqoom
Kitabu kilicho andikwa.
- 21
يَشْهَدُهُ ٱلْمُقَرَّبُونَ
Unukuzi: Yashhadu hul muqarra boon
Wanakishuhudia walio karibishwa.
- 22
إِنَّ ٱلْأَبْرَارَ لَفِى نَعِيمٍ
Unukuzi: Innal abraara lafee Na'eem
Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.
- 23
عَلَى ٱلْأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ
Unukuzi: 'Alal araaa'iki yanzuroon
Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.
- 24
تَعْرِفُ فِى وُجُوهِهِمْ نَضْرَةَ ٱلنَّعِيمِ
Unukuzi: Ta'rifu fee wujoohihim nadratan na'eem
Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,
- 25
يُسْقَوْنَ مِن رَّحِيقٍۢ مَّخْتُومٍ
Unukuzi: Yusqawna mir raheeqim makhtoom
Watanyweshwa kinywaji safi kiliyo tiwa muhuri,
- 26
خِتَٰمُهُۥ مِسْكٌۭ ۚ وَفِى ذَٰلِكَ فَلْيَتَنَافَسِ ٱلْمُتَنَٰفِسُونَ
Unukuzi: Khitaamuhoo misk; wa fee zaalika falyatanaafasil Mutanaafisoon
Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana.
- 27
وَمِزَاجُهُۥ مِن تَسْنِيمٍ
Unukuzi: Wa mizaajuhoo min Tasneem
Na mchanganyiko wake ni Tasniim,
- 28
عَيْنًۭا يَشْرَبُ بِهَا ٱلْمُقَرَّبُونَ
Unukuzi: 'Ainaiy yashrabu bihal muqarraboon
Chemchem watakayo inywa walio kurubishwa.
- 29
إِنَّ ٱلَّذِينَ أَجْرَمُوا۟ كَانُوا۟ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ يَضْحَكُونَ
Unukuzi: Innal lazeena ajramoo kaanoo minal lazeena aamanoo yadhakoon
Kwa hakika wale walio kuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walio amini.
- 30
وَإِذَا مَرُّوا۟ بِهِمْ يَتَغَامَزُونَ
Unukuzi: Wa izaa marroo bihim yataghaamazoon
Na wanapo pita karibu yao wakikonyezana.
- 31
وَإِذَا ٱنقَلَبُوٓا۟ إِلَىٰٓ أَهْلِهِمُ ٱنقَلَبُوا۟ فَكِهِينَ
Unukuzi: Wa izan qalabooo ilaaa ahlihimun qalaboo fakiheen
Na wanapo rudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi.
- 32
وَإِذَا رَأَوْهُمْ قَالُوٓا۟ إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ لَضَآلُّونَ
Unukuzi: Wa izaa ra awhum qaalooo inna haaa'ulaaa'i ladaaal loon
Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea.
- 33
وَمَآ أُرْسِلُوا۟ عَلَيْهِمْ حَٰفِظِينَ
Unukuzi: Wa maaa ursiloo 'alaihim haafizeen
Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao.
- 34
فَٱلْيَوْمَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ مِنَ ٱلْكُفَّارِ يَضْحَكُونَ
Unukuzi: Fal yawmal lazeena aamanoo minal kuffaari yadhakoon
Basi leo walio amini ndio watawacheka makafiri,
- 35
عَلَى ٱلْأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ
Unukuzi: 'Alal araaa'iki yanzuroon
Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.
- 36
هَلْ ثُوِّبَ ٱلْكُفَّارُ مَا كَانُوا۟ يَفْعَلُونَ
Unukuzi: Hal suwwibal kuffaaru maa kaanoo yaf'aloon
Je! makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda?
Toleo la tafsiri: sw.barwani
Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).
Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.
Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.