Sura zote

Surah 83

The Defrauding

سُورَةُ المُطَفِّفِينَ

Al-Mutaffifin · Makka

Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia

Sauti
  1. 1

    بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَيْلٌۭ لِّلْمُطَفِّفِينَ

    Unukuzi: Wailul lil mutaffifeen

    Ole wao hao wapunjao!

  2. 2

    ٱلَّذِينَ إِذَا ٱكْتَالُوا۟ عَلَى ٱلنَّاسِ يَسْتَوْفُونَ

    Unukuzi: Allazeena izak taaloo 'alan naasi yastawfoon

    Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.

  3. 3

    وَإِذَا كَالُوهُمْ أَو وَّزَنُوهُمْ يُخْسِرُونَ

    Unukuzi: Wa izaa kaaloohum aw wazanoohum yukhsiroon

    Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.

  4. 4

    أَلَا يَظُنُّ أُو۟لَٰٓئِكَ أَنَّهُم مَّبْعُوثُونَ

    Unukuzi: Alaa yazunnu ulaaa'ika annahum mab'oosoon

    Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa

  5. 5

    لِيَوْمٍ عَظِيمٍۢ

    Unukuzi: Li Yawmin 'Azeem

    Katika Siku iliyo kuu,

  6. 6

    يَوْمَ يَقُومُ ٱلنَّاسُ لِرَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ

    Unukuzi: Yawma yaqoomun naasu li Rabbil 'aalameen

    Siku watapo msimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?

  7. 7

    كَلَّآ إِنَّ كِتَٰبَ ٱلْفُجَّارِ لَفِى سِجِّينٍۢ

    Unukuzi: Kallaaa inna kitaabal fujjaari lafee Sijjeen

    Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.

  8. 8

    وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا سِجِّينٌۭ

    Unukuzi: Wa maa adraaka maa Sijjeen

    Unajua nini Sijjin?

  9. 9

    كِتَٰبٌۭ مَّرْقُومٌۭ

    Unukuzi: Kitaabum marqoom

    Kitabu kilicho andikwa.

  10. 10

    وَيْلٌۭ يَوْمَئِذٍۢ لِّلْمُكَذِّبِينَ

    Unukuzi: Wailuny yawma'izil lil mukazzibeen

    Ole wao siku hiyo kwa wanao kadhibisha!

  11. 11

    ٱلَّذِينَ يُكَذِّبُونَ بِيَوْمِ ٱلدِّينِ

    Unukuzi: Allazeena yukazziboona bi yawmid deen

    Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.

  12. 12

    وَمَا يُكَذِّبُ بِهِۦٓ إِلَّا كُلُّ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ

    Unukuzi: Wa maa yukazzibu biheee illaa kullu mu'tadin aseem

    Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.

  13. 13

    إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ ءَايَٰتُنَا قَالَ أَسَٰطِيرُ ٱلْأَوَّلِينَ

    Unukuzi: Izaa tutlaa'alaihi aayaatunaa qaala asaateerul awwaleen

    Anapo somewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale!

  14. 14

    كَلَّا ۖ بَلْ ۜ رَانَ عَلَىٰ قُلُوبِهِم مَّا كَانُوا۟ يَكْسِبُونَ

    Unukuzi: Kallaa bal raana 'alaa quloobihim maa kaanoo yaksiboon

    Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao walio kuwa wakiyachuma.

  15. 15

    كَلَّآ إِنَّهُمْ عَن رَّبِّهِمْ يَوْمَئِذٍۢ لَّمَحْجُوبُونَ

    Unukuzi: Kallaaa innahum 'ar Rabbihim yawma'izil lamah jooboon

    Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi.

  16. 16

    ثُمَّ إِنَّهُمْ لَصَالُوا۟ ٱلْجَحِيمِ

    Unukuzi: Summa innahum lasaa lul jaheem

    Kisha wataingia Motoni!

  17. 17

    ثُمَّ يُقَالُ هَٰذَا ٱلَّذِى كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ

    Unukuzi: Summa yuqaalu haazal lazee kuntum bihee tukazziboon

    Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyakadhabisha.

  18. 18

    كَلَّآ إِنَّ كِتَٰبَ ٱلْأَبْرَارِ لَفِى عِلِّيِّينَ

    Unukuzi: Kallaaa inna kitaabal abraari lafee'Illiyyeen

    Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I'liyyin.

  19. 19

    وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا عِلِّيُّونَ

    Unukuzi: Wa maaa adraaka maa 'Illiyyoon

    Na nini kitakacho kujuvya nini I'liyyin?

  20. 20

    كِتَٰبٌۭ مَّرْقُومٌۭ

    Unukuzi: Kitaabum marqoom

    Kitabu kilicho andikwa.

  21. 21

    يَشْهَدُهُ ٱلْمُقَرَّبُونَ

    Unukuzi: Yashhadu hul muqarra boon

    Wanakishuhudia walio karibishwa.

  22. 22

    إِنَّ ٱلْأَبْرَارَ لَفِى نَعِيمٍ

    Unukuzi: Innal abraara lafee Na'eem

    Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.

  23. 23

    عَلَى ٱلْأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ

    Unukuzi: 'Alal araaa'iki yanzuroon

    Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.

  24. 24

    تَعْرِفُ فِى وُجُوهِهِمْ نَضْرَةَ ٱلنَّعِيمِ

    Unukuzi: Ta'rifu fee wujoohihim nadratan na'eem

    Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,

  25. 25

    يُسْقَوْنَ مِن رَّحِيقٍۢ مَّخْتُومٍ

    Unukuzi: Yusqawna mir raheeqim makhtoom

    Watanyweshwa kinywaji safi kiliyo tiwa muhuri,

  26. 26

    خِتَٰمُهُۥ مِسْكٌۭ ۚ وَفِى ذَٰلِكَ فَلْيَتَنَافَسِ ٱلْمُتَنَٰفِسُونَ

    Unukuzi: Khitaamuhoo misk; wa fee zaalika falyatanaafasil Mutanaafisoon

    Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana.

  27. 27

    وَمِزَاجُهُۥ مِن تَسْنِيمٍ

    Unukuzi: Wa mizaajuhoo min Tasneem

    Na mchanganyiko wake ni Tasniim,

  28. 28

    عَيْنًۭا يَشْرَبُ بِهَا ٱلْمُقَرَّبُونَ

    Unukuzi: 'Ainaiy yashrabu bihal muqarraboon

    Chemchem watakayo inywa walio kurubishwa.

  29. 29

    إِنَّ ٱلَّذِينَ أَجْرَمُوا۟ كَانُوا۟ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ يَضْحَكُونَ

    Unukuzi: Innal lazeena ajramoo kaanoo minal lazeena aamanoo yadhakoon

    Kwa hakika wale walio kuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walio amini.

  30. 30

    وَإِذَا مَرُّوا۟ بِهِمْ يَتَغَامَزُونَ

    Unukuzi: Wa izaa marroo bihim yataghaamazoon

    Na wanapo pita karibu yao wakikonyezana.

  31. 31

    وَإِذَا ٱنقَلَبُوٓا۟ إِلَىٰٓ أَهْلِهِمُ ٱنقَلَبُوا۟ فَكِهِينَ

    Unukuzi: Wa izan qalabooo ilaaa ahlihimun qalaboo fakiheen

    Na wanapo rudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi.

  32. 32

    وَإِذَا رَأَوْهُمْ قَالُوٓا۟ إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ لَضَآلُّونَ

    Unukuzi: Wa izaa ra awhum qaalooo inna haaa'ulaaa'i ladaaal loon

    Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea.

  33. 33

    وَمَآ أُرْسِلُوا۟ عَلَيْهِمْ حَٰفِظِينَ

    Unukuzi: Wa maaa ursiloo 'alaihim haafizeen

    Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao.

  34. 34

    فَٱلْيَوْمَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ مِنَ ٱلْكُفَّارِ يَضْحَكُونَ

    Unukuzi: Fal yawmal lazeena aamanoo minal kuffaari yadhakoon

    Basi leo walio amini ndio watawacheka makafiri,

  35. 35

    عَلَى ٱلْأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ

    Unukuzi: 'Alal araaa'iki yanzuroon

    Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.

  36. 36

    هَلْ ثُوِّبَ ٱلْكُفَّارُ مَا كَانُوا۟ يَفْعَلُونَ

    Unukuzi: Hal suwwibal kuffaaru maa kaanoo yaf'aloon

    Je! makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda?

Toleo la tafsiri: sw.barwani

Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).

Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.

Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.

The Defrauding — Islam Word