Sura zote

Surah 82

The Cleaving

سُورَةُ الانفِطَارِ

Al-Infitaar · Makka

Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia

Sauti
  1. 1

    بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنفَطَرَتْ

    Unukuzi: Izas samaaa'un fatarat

    Mbingu itapo chanika,

  2. 2

    وَإِذَا ٱلْكَوَاكِبُ ٱنتَثَرَتْ

    Unukuzi: Wa izal kawaakibun tasarat

    Na nyota zitapo tawanyika,

  3. 3

    وَإِذَا ٱلْبِحَارُ فُجِّرَتْ

    Unukuzi: Wa izal bihaaru fujjirat

    Na bahari zitakapo pasuliwa,

  4. 4

    وَإِذَا ٱلْقُبُورُ بُعْثِرَتْ

    Unukuzi: Wa izal qubooru bu'sirat

    Na makaburi yatapo fukuliwa,

  5. 5

    عَلِمَتْ نَفْسٌۭ مَّا قَدَّمَتْ وَأَخَّرَتْ

    Unukuzi: 'Alimat nafsum maa qaddamat wa akhkharat

    Hapo kila nafsi itajua ilicho tanguliza, na ilicho bakisha nyuma.

  6. 6

    يَٰٓأَيُّهَا ٱلْإِنسَٰنُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ ٱلْكَرِيمِ

    Unukuzi: Yaaa ayyuhal insaaanu maa gharraka bi Rabbikal kareem

    Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?

  7. 7

    ٱلَّذِى خَلَقَكَ فَسَوَّىٰكَ فَعَدَلَكَ

    Unukuzi: Allazee khalaqaka fasaw waaka fa'adalak

    Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha,

  8. 8

    فِىٓ أَىِّ صُورَةٍۢ مَّا شَآءَ رَكَّبَكَ

    Unukuzi: Feee ayye sooratim maa shaaa'a rakkabak

    Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga.

  9. 9

    كَلَّا بَلْ تُكَذِّبُونَ بِٱلدِّينِ

    Unukuzi: Kalla bal tukazziboona bid deen

    Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo.

  10. 10

    وَإِنَّ عَلَيْكُمْ لَحَٰفِظِينَ

    Unukuzi: Wa inna 'alaikum lahaa fizeen

    Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,

  11. 11

    كِرَامًۭا كَٰتِبِينَ

    Unukuzi: Kiraaman kaatibeen

    Waandishi wenye hishima,

  12. 12

    يَعْلَمُونَ مَا تَفْعَلُونَ

    Unukuzi: Ya'lamoona ma taf'aloon

    Wanayajua mnayo yatenda.

  13. 13

    إِنَّ ٱلْأَبْرَارَ لَفِى نَعِيمٍۢ

    Unukuzi: Innal abraara lafee na'eem

    Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema,

  14. 14

    وَإِنَّ ٱلْفُجَّارَ لَفِى جَحِيمٍۢ

    Unukuzi: Wa innal fujjaara lafee jaheem

    Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;

  15. 15

    يَصْلَوْنَهَا يَوْمَ ٱلدِّينِ

    Unukuzi: Yaslawnahaa Yawmad Deen

    Wataingia humo Siku ya Malipo.

  16. 16

    وَمَا هُمْ عَنْهَا بِغَآئِبِينَ

    Unukuzi: Wa maa hum 'anhaa bighaaa 'ibeen

    Na hawatoacha kuwamo humo.

  17. 17

    وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا يَوْمُ ٱلدِّينِ

    Unukuzi: Wa maaa adraaka maa Yawmud Deen

    Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?

  18. 18

    ثُمَّ مَآ أَدْرَىٰكَ مَا يَوْمُ ٱلدِّينِ

    Unukuzi: Summa maaa adraaka maa Yawmud Deen

    Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?

  19. 19

    يَوْمَ لَا تَمْلِكُ نَفْسٌۭ لِّنَفْسٍۢ شَيْـًۭٔا ۖ وَٱلْأَمْرُ يَوْمَئِذٍۢ لِّلَّهِ

    Unukuzi: Yawma laa tamliku nafsul linafsin shai'anw walamru yawma'izil lillaah

    Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.

Toleo la tafsiri: sw.barwani

Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).

Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.

Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.

The Cleaving — Islam Word