Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia
- 1
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنفَطَرَتْ
Unukuzi: Izas samaaa'un fatarat
Mbingu itapo chanika,
- 2
وَإِذَا ٱلْكَوَاكِبُ ٱنتَثَرَتْ
Unukuzi: Wa izal kawaakibun tasarat
Na nyota zitapo tawanyika,
- 3
وَإِذَا ٱلْبِحَارُ فُجِّرَتْ
Unukuzi: Wa izal bihaaru fujjirat
Na bahari zitakapo pasuliwa,
- 4
وَإِذَا ٱلْقُبُورُ بُعْثِرَتْ
Unukuzi: Wa izal qubooru bu'sirat
Na makaburi yatapo fukuliwa,
- 5
عَلِمَتْ نَفْسٌۭ مَّا قَدَّمَتْ وَأَخَّرَتْ
Unukuzi: 'Alimat nafsum maa qaddamat wa akhkharat
Hapo kila nafsi itajua ilicho tanguliza, na ilicho bakisha nyuma.
- 6
يَٰٓأَيُّهَا ٱلْإِنسَٰنُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ ٱلْكَرِيمِ
Unukuzi: Yaaa ayyuhal insaaanu maa gharraka bi Rabbikal kareem
Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?
- 7
ٱلَّذِى خَلَقَكَ فَسَوَّىٰكَ فَعَدَلَكَ
Unukuzi: Allazee khalaqaka fasaw waaka fa'adalak
Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha,
- 8
فِىٓ أَىِّ صُورَةٍۢ مَّا شَآءَ رَكَّبَكَ
Unukuzi: Feee ayye sooratim maa shaaa'a rakkabak
Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga.
- 9
كَلَّا بَلْ تُكَذِّبُونَ بِٱلدِّينِ
Unukuzi: Kalla bal tukazziboona bid deen
Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo.
- 10
وَإِنَّ عَلَيْكُمْ لَحَٰفِظِينَ
Unukuzi: Wa inna 'alaikum lahaa fizeen
Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,
- 11
كِرَامًۭا كَٰتِبِينَ
Unukuzi: Kiraaman kaatibeen
Waandishi wenye hishima,
- 12
يَعْلَمُونَ مَا تَفْعَلُونَ
Unukuzi: Ya'lamoona ma taf'aloon
Wanayajua mnayo yatenda.
- 13
إِنَّ ٱلْأَبْرَارَ لَفِى نَعِيمٍۢ
Unukuzi: Innal abraara lafee na'eem
Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema,
- 14
وَإِنَّ ٱلْفُجَّارَ لَفِى جَحِيمٍۢ
Unukuzi: Wa innal fujjaara lafee jaheem
Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;
- 15
يَصْلَوْنَهَا يَوْمَ ٱلدِّينِ
Unukuzi: Yaslawnahaa Yawmad Deen
Wataingia humo Siku ya Malipo.
- 16
وَمَا هُمْ عَنْهَا بِغَآئِبِينَ
Unukuzi: Wa maa hum 'anhaa bighaaa 'ibeen
Na hawatoacha kuwamo humo.
- 17
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا يَوْمُ ٱلدِّينِ
Unukuzi: Wa maaa adraaka maa Yawmud Deen
Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
- 18
ثُمَّ مَآ أَدْرَىٰكَ مَا يَوْمُ ٱلدِّينِ
Unukuzi: Summa maaa adraaka maa Yawmud Deen
Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
- 19
يَوْمَ لَا تَمْلِكُ نَفْسٌۭ لِّنَفْسٍۢ شَيْـًۭٔا ۖ وَٱلْأَمْرُ يَوْمَئِذٍۢ لِّلَّهِ
Unukuzi: Yawma laa tamliku nafsul linafsin shai'anw walamru yawma'izil lillaah
Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.
Toleo la tafsiri: sw.barwani
Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).
Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.
Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.