Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia
- 1
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ إِذَا ٱلشَّمْسُ كُوِّرَتْ
Unukuzi: Izash shamsu kuwwirat
Jua litakapo kunjwa,
- 2
وَإِذَا ٱلنُّجُومُ ٱنكَدَرَتْ
Unukuzi: Wa izan nujoomun kadarat
Na nyota zikazimwa,
- 3
وَإِذَا ٱلْجِبَالُ سُيِّرَتْ
Unukuzi: Wa izal jibaalu suyyirat
Na milima ikaondolewa,
- 4
وَإِذَا ٱلْعِشَارُ عُطِّلَتْ
Unukuzi: Wa izal 'ishaaru 'uttilat
Na ngamia wenye mimba pevu watakapo achwa wasishughulikiwe,
- 5
وَإِذَا ٱلْوُحُوشُ حُشِرَتْ
Unukuzi: Wa izal wuhooshu hushirat
Na wanyama wa mwituni wakakusanywa,
- 6
وَإِذَا ٱلْبِحَارُ سُجِّرَتْ
Unukuzi: Wa izal bihaaru sujjirat
Na bahari zikawaka moto,
- 7
وَإِذَا ٱلنُّفُوسُ زُوِّجَتْ
Unukuzi: Wa izan nufoosu zuwwijat
Na nafsi zikaunganishwa,
- 8
وَإِذَا ٱلْمَوْءُۥدَةُ سُئِلَتْ
Unukuzi: Wa izal maw'oodatu su'ilat
Na msichana aliye zikwa hai atapo ulizwa,
- 9
بِأَىِّ ذَنۢبٍۢ قُتِلَتْ
Unukuzi: Bi ayyi zambin qutilat
Kwa kosa gani aliuliwa?
- 10
وَإِذَا ٱلصُّحُفُ نُشِرَتْ
Unukuzi: Wa izas suhufu nushirat
Na madaftari yatakapo enezwa,
- 11
وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ كُشِطَتْ
Unukuzi: Wa izas samaaa'u kushitat
Na mbingu itapo tanduliwa,
- 12
وَإِذَا ٱلْجَحِيمُ سُعِّرَتْ
Unukuzi: Wa izal jaheemu su'-'irat
Na Jahannamu itapo chochewa,
- 13
وَإِذَا ٱلْجَنَّةُ أُزْلِفَتْ
Unukuzi: Wa izal jannatu uzlifat
Na Pepo ikasogezwa,
- 14
عَلِمَتْ نَفْسٌۭ مَّآ أَحْضَرَتْ
Unukuzi: 'Alimat nafsum maaa ahdarat
Kila nafsi itajua ilicho kihudhurisha.
- 15
فَلَآ أُقْسِمُ بِٱلْخُنَّسِ
Unukuzi: Falaaa uqsimu bil khunnas
Naapa kwa nyota zinapo rejea nyuma,
- 16
ٱلْجَوَارِ ٱلْكُنَّسِ
Unukuzi: Al jawaaril kunnas
Zinazo kwenda, kisha zikajificha,
- 17
وَٱلَّيْلِ إِذَا عَسْعَسَ
Unukuzi: Wallaili izaa 'as'as
Na kwa usiku unapo pungua,
- 18
وَٱلصُّبْحِ إِذَا تَنَفَّسَ
Unukuzi: Wassubhi izaa tanaffas
Na kwa asubuhi inapo pambazuka,
- 19
إِنَّهُۥ لَقَوْلُ رَسُولٍۢ كَرِيمٍۢ
Unukuzi: Innahoo laqawlu rasoolin kareem
Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu,
- 20
ذِى قُوَّةٍ عِندَ ذِى ٱلْعَرْشِ مَكِينٍۢ
Unukuzi: Zee quwwatin 'inda zil 'arshi makeen
Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi,
- 21
مُّطَاعٍۢ ثَمَّ أَمِينٍۢ
Unukuzi: Mutaa'in samma ameen
Anaye t'iiwa, tena muaminifu.
- 22
وَمَا صَاحِبُكُم بِمَجْنُونٍۢ
Unukuzi: Wa maa saahibukum bimajnoon
Na wala huyu mwenzenu hana wazimu.
- 23
وَلَقَدْ رَءَاهُ بِٱلْأُفُقِ ٱلْمُبِينِ
Unukuzi: Wa laqad ra aahu bilufuqil mubeen
Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi.
- 24
وَمَا هُوَ عَلَى ٱلْغَيْبِ بِضَنِينٍۢ
Unukuzi: Wa maa huwa 'alal ghaibi bidaneen
Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu.
- 25
وَمَا هُوَ بِقَوْلِ شَيْطَٰنٍۢ رَّجِيمٍۢ
Unukuzi: Wa maa huwa biqawli shaitaanir rajeem
Wala hii si kauli ya Shetani maluuni.
- 26
فَأَيْنَ تَذْهَبُونَ
Unukuzi: Fa ayna tazhaboon
Basi mnakwenda wapi?
- 27
إِنْ هُوَ إِلَّا ذِكْرٌۭ لِّلْعَٰلَمِينَ
Unukuzi: In huwa illaa zikrul lil'aalameen
Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
- 28
لِمَن شَآءَ مِنكُمْ أَن يَسْتَقِيمَ
Unukuzi: Liman shaaa'a minkum ai yastaqeem
Kwa yule miongoni mwenu anaye taka kwenda sawa.
- 29
وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ رَبُّ ٱلْعَٰلَمِينَ
Unukuzi: Wa maa tashaaa'oona illaaa ai yashaaa 'al laahu Rabbul 'Aalameen
Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Toleo la tafsiri: sw.barwani
Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).
Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.
Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.