Sura zote

Surah 81

The Overthrowing

سُورَةُ التَّكۡوِيرِ

At-Takwir · Makka

Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia

Sauti
  1. 1

    بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ إِذَا ٱلشَّمْسُ كُوِّرَتْ

    Unukuzi: Izash shamsu kuwwirat

    Jua litakapo kunjwa,

  2. 2

    وَإِذَا ٱلنُّجُومُ ٱنكَدَرَتْ

    Unukuzi: Wa izan nujoomun kadarat

    Na nyota zikazimwa,

  3. 3

    وَإِذَا ٱلْجِبَالُ سُيِّرَتْ

    Unukuzi: Wa izal jibaalu suyyirat

    Na milima ikaondolewa,

  4. 4

    وَإِذَا ٱلْعِشَارُ عُطِّلَتْ

    Unukuzi: Wa izal 'ishaaru 'uttilat

    Na ngamia wenye mimba pevu watakapo achwa wasishughulikiwe,

  5. 5

    وَإِذَا ٱلْوُحُوشُ حُشِرَتْ

    Unukuzi: Wa izal wuhooshu hushirat

    Na wanyama wa mwituni wakakusanywa,

  6. 6

    وَإِذَا ٱلْبِحَارُ سُجِّرَتْ

    Unukuzi: Wa izal bihaaru sujjirat

    Na bahari zikawaka moto,

  7. 7

    وَإِذَا ٱلنُّفُوسُ زُوِّجَتْ

    Unukuzi: Wa izan nufoosu zuwwijat

    Na nafsi zikaunganishwa,

  8. 8

    وَإِذَا ٱلْمَوْءُۥدَةُ سُئِلَتْ

    Unukuzi: Wa izal maw'oodatu su'ilat

    Na msichana aliye zikwa hai atapo ulizwa,

  9. 9

    بِأَىِّ ذَنۢبٍۢ قُتِلَتْ

    Unukuzi: Bi ayyi zambin qutilat

    Kwa kosa gani aliuliwa?

  10. 10

    وَإِذَا ٱلصُّحُفُ نُشِرَتْ

    Unukuzi: Wa izas suhufu nushirat

    Na madaftari yatakapo enezwa,

  11. 11

    وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ كُشِطَتْ

    Unukuzi: Wa izas samaaa'u kushitat

    Na mbingu itapo tanduliwa,

  12. 12

    وَإِذَا ٱلْجَحِيمُ سُعِّرَتْ

    Unukuzi: Wa izal jaheemu su'-'irat

    Na Jahannamu itapo chochewa,

  13. 13

    وَإِذَا ٱلْجَنَّةُ أُزْلِفَتْ

    Unukuzi: Wa izal jannatu uzlifat

    Na Pepo ikasogezwa,

  14. 14

    عَلِمَتْ نَفْسٌۭ مَّآ أَحْضَرَتْ

    Unukuzi: 'Alimat nafsum maaa ahdarat

    Kila nafsi itajua ilicho kihudhurisha.

  15. 15

    فَلَآ أُقْسِمُ بِٱلْخُنَّسِ

    Unukuzi: Falaaa uqsimu bil khunnas

    Naapa kwa nyota zinapo rejea nyuma,

  16. 16

    ٱلْجَوَارِ ٱلْكُنَّسِ

    Unukuzi: Al jawaaril kunnas

    Zinazo kwenda, kisha zikajificha,

  17. 17

    وَٱلَّيْلِ إِذَا عَسْعَسَ

    Unukuzi: Wallaili izaa 'as'as

    Na kwa usiku unapo pungua,

  18. 18

    وَٱلصُّبْحِ إِذَا تَنَفَّسَ

    Unukuzi: Wassubhi izaa tanaffas

    Na kwa asubuhi inapo pambazuka,

  19. 19

    إِنَّهُۥ لَقَوْلُ رَسُولٍۢ كَرِيمٍۢ

    Unukuzi: Innahoo laqawlu rasoolin kareem

    Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu,

  20. 20

    ذِى قُوَّةٍ عِندَ ذِى ٱلْعَرْشِ مَكِينٍۢ

    Unukuzi: Zee quwwatin 'inda zil 'arshi makeen

    Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi,

  21. 21

    مُّطَاعٍۢ ثَمَّ أَمِينٍۢ

    Unukuzi: Mutaa'in samma ameen

    Anaye t'iiwa, tena muaminifu.

  22. 22

    وَمَا صَاحِبُكُم بِمَجْنُونٍۢ

    Unukuzi: Wa maa saahibukum bimajnoon

    Na wala huyu mwenzenu hana wazimu.

  23. 23

    وَلَقَدْ رَءَاهُ بِٱلْأُفُقِ ٱلْمُبِينِ

    Unukuzi: Wa laqad ra aahu bilufuqil mubeen

    Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi.

  24. 24

    وَمَا هُوَ عَلَى ٱلْغَيْبِ بِضَنِينٍۢ

    Unukuzi: Wa maa huwa 'alal ghaibi bidaneen

    Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu.

  25. 25

    وَمَا هُوَ بِقَوْلِ شَيْطَٰنٍۢ رَّجِيمٍۢ

    Unukuzi: Wa maa huwa biqawli shaitaanir rajeem

    Wala hii si kauli ya Shetani maluuni.

  26. 26

    فَأَيْنَ تَذْهَبُونَ

    Unukuzi: Fa ayna tazhaboon

    Basi mnakwenda wapi?

  27. 27

    إِنْ هُوَ إِلَّا ذِكْرٌۭ لِّلْعَٰلَمِينَ

    Unukuzi: In huwa illaa zikrul lil'aalameen

    Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.

  28. 28

    لِمَن شَآءَ مِنكُمْ أَن يَسْتَقِيمَ

    Unukuzi: Liman shaaa'a minkum ai yastaqeem

    Kwa yule miongoni mwenu anaye taka kwenda sawa.

  29. 29

    وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ رَبُّ ٱلْعَٰلَمِينَ

    Unukuzi: Wa maa tashaaa'oona illaaa ai yashaaa 'al laahu Rabbul 'Aalameen

    Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Toleo la tafsiri: sw.barwani

Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).

Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.

Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.