Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia
- 1
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ عَبَسَ وَتَوَلَّىٰٓ
Unukuzi: 'Abasa wa tawallaa.
Alikunja kipaji na akageuka,
- 2
أَن جَآءَهُ ٱلْأَعْمَىٰ
Unukuzi: An jaa-ahul 'a-maa
Kwa sababu alimjia kipofu!
- 3
وَمَا يُدْرِيكَ لَعَلَّهُۥ يَزَّكَّىٰٓ
Unukuzi: Wa maa yudreeka la'allahu yaz zakkaa.
Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika?
- 4
أَوْ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ ٱلذِّكْرَىٰٓ
Unukuzi: Au yaz zak karu fatanfa 'ahuz zikraa.
Au atawaidhika, na mawaidha yamfae?
- 5
أَمَّا مَنِ ٱسْتَغْنَىٰ
Unukuzi: Amma manis taghnaa
Ama ajionaye hana haja,
- 6
فَأَنتَ لَهُۥ تَصَدَّىٰ
Unukuzi: Fa-anta lahu tasaddaa
Wewe ndio unamshughulikia?
- 7
وَمَا عَلَيْكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ
Unukuzi: Wa ma 'alaika allaa yaz zakka.
Na si juu yako kama hakutakasika.
- 8
وَأَمَّا مَن جَآءَكَ يَسْعَىٰ
Unukuzi: Wa amma man jaa-aka yas'a
Ama anaye kujia kwa juhudi,
- 9
وَهُوَ يَخْشَىٰ
Unukuzi: Wahuwa yakhshaa,
Naye anaogopa,
- 10
فَأَنتَ عَنْهُ تَلَهَّىٰ
Unukuzi: Fa-anta 'anhu talah haa.
Ndio wewe unampuuza?
- 11
كَلَّآ إِنَّهَا تَذْكِرَةٌۭ
Unukuzi: Kalla innaha tazkirah
Sivyo hivyo! Huku ni kukumbushana.
- 12
فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ
Unukuzi: Faman shaa a zakarah
Basi anaye penda akumbuke.
- 13
فِى صُحُفٍۢ مُّكَرَّمَةٍۢ
Unukuzi: Fi suhufim mukar rama,
Yamo katika kurasa zilizo hishimiwa,
- 14
مَّرْفُوعَةٍۢ مُّطَهَّرَةٍۭ
Unukuzi: Marfoo'atim mutah hara,
Zilizo inuliwa, zilizo takaswa.
- 15
بِأَيْدِى سَفَرَةٍۢ
Unukuzi: Bi'aidee safara
Zimo mikononi mwa Malaika waandishi,
- 16
كِرَامٍۭ بَرَرَةٍۢ
Unukuzi: Kiraamim bararah.
Watukufu, wema.
- 17
قُتِلَ ٱلْإِنسَٰنُ مَآ أَكْفَرَهُۥ
Unukuzi: Qutilal-insanu maa akfarah.
Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha?
- 18
مِنْ أَىِّ شَىْءٍ خَلَقَهُۥ
Unukuzi: Min aiyyi shai-in Khalaq
Kwa kitu gani amemuumba?
- 19
مِن نُّطْفَةٍ خَلَقَهُۥ فَقَدَّرَهُۥ
Unukuzi: Min nutfah; khalaqahu faqad-darah.
Kwa tone la manii, akamuumba na akamkadiria.
- 20
ثُمَّ ٱلسَّبِيلَ يَسَّرَهُۥ
Unukuzi: Thummas sabeela yas-sarah
Kisha akamsahilishia njia.
- 21
ثُمَّ أَمَاتَهُۥ فَأَقْبَرَهُۥ
Unukuzi: Thumma amatahu fa-aqbarah
Kisha akamfisha, akamtia kaburini.
- 22
ثُمَّ إِذَا شَآءَ أَنشَرَهُۥ
Unukuzi: Thumma iza shaa-a ansharah
Kisha apendapo atamfufua.
- 23
كَلَّا لَمَّا يَقْضِ مَآ أَمَرَهُۥ
Unukuzi: Kalla lamma yaqdi maa amarah.
La! Hajamaliza aliyo muamuru.
- 24
فَلْيَنظُرِ ٱلْإِنسَٰنُ إِلَىٰ طَعَامِهِۦٓ
Unukuzi: Falyanzuril insanu ilaa ta-amih
Hebu mtu na atazame chakula chake.
- 25
أَنَّا صَبَبْنَا ٱلْمَآءَ صَبًّۭا
Unukuzi: Anna sabab nalmaa-a sabba.
Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu,
- 26
ثُمَّ شَقَقْنَا ٱلْأَرْضَ شَقًّۭا
Unukuzi: Thumma sha qaqnal-arda shaqqa.
Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu,
- 27
فَأَنۢبَتْنَا فِيهَا حَبًّۭا
Unukuzi: Fa ambatna feeha habba
Kisha tukaotesha humo nafaka,
- 28
وَعِنَبًۭا وَقَضْبًۭا
Unukuzi: Wa 'inabaw-wa qadba
Na zabibu, na mimea ya majani,
- 29
وَزَيْتُونًۭا وَنَخْلًۭا
Unukuzi: Wa zaitoonaw wanakh la'
Na mizaituni, na mitende,
- 30
وَحَدَآئِقَ غُلْبًۭا
Unukuzi: Wa hadaa-iqa ghulba
Na bustani zenye miti iliyo songana baraabara,
- 31
وَفَٰكِهَةًۭ وَأَبًّۭا
Unukuzi: Wa faki hataw-wa abba.
Na matunda, na malisho ya wanyama;
- 32
مَّتَٰعًۭا لَّكُمْ وَلِأَنْعَٰمِكُمْ
Unukuzi: Mata'al-lakum wa li-an'amikum.
Kwa manufaa yenu na mifugo yenu.
- 33
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلصَّآخَّةُ
Unukuzi: Faiza jaa-atis saakhah.
Basi utakapo kuja ukelele,
- 34
يَوْمَ يَفِرُّ ٱلْمَرْءُ مِنْ أَخِيهِ
Unukuzi: Yauma yafir-rul mar-u min akheeh
Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye,
- 35
وَأُمِّهِۦ وَأَبِيهِ
Unukuzi: Wa ummihee wa abeeh
Na mamaye na babaye,
- 36
وَصَٰحِبَتِهِۦ وَبَنِيهِ
Unukuzi: Wa sahi batihee wa baneeh.
Na mkewe na wanawe -
- 37
لِكُلِّ ٱمْرِئٍۢ مِّنْهُمْ يَوْمَئِذٍۢ شَأْنٌۭ يُغْنِيهِ
Unukuzi: Likul limri-im-minuhm yaumaa-izin shaa nuy-yughneeh
Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha.
- 38
وُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍۢ مُّسْفِرَةٌۭ
Unukuzi: Wujoo huny-yauma-izim-musfira;
Siku hiyo ziko nyuso zitazo nawiri,
- 39
ضَاحِكَةٌۭ مُّسْتَبْشِرَةٌۭ
Unukuzi: Dahi katum mustab shirah
Zitacheka, zitachangamka;
- 40
وَوُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍ عَلَيْهَا غَبَرَةٌۭ
Unukuzi: Wa wujoohuy yauma-izin 'alaiha ghabar a
Na nyuso siku hiyo zitakuwa na mavumbi,
- 41
تَرْهَقُهَا قَتَرَةٌ
Unukuzi: Tarhaquha qatarah.
Giza totoro litazifunika,
- 42
أُو۟لَٰٓئِكَ هُمُ ٱلْكَفَرَةُ ٱلْفَجَرَةُ
Unukuzi: Ulaa-ika humul-kafa ratul-fajarah.
Hao ndio makafiri watenda maovu.
Toleo la tafsiri: sw.barwani
Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).
Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.
Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.