Sura zote

Surah 80

He Frowned

سُورَةُ عَبَسَ

Abasa · Makka

Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia

Sauti
  1. 1

    بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ عَبَسَ وَتَوَلَّىٰٓ

    Unukuzi: 'Abasa wa tawallaa.

    Alikunja kipaji na akageuka,

  2. 2

    أَن جَآءَهُ ٱلْأَعْمَىٰ

    Unukuzi: An jaa-ahul 'a-maa

    Kwa sababu alimjia kipofu!

  3. 3

    وَمَا يُدْرِيكَ لَعَلَّهُۥ يَزَّكَّىٰٓ

    Unukuzi: Wa maa yudreeka la'allahu yaz zakkaa.

    Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika?

  4. 4

    أَوْ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ ٱلذِّكْرَىٰٓ

    Unukuzi: Au yaz zak karu fatanfa 'ahuz zikraa.

    Au atawaidhika, na mawaidha yamfae?

  5. 5

    أَمَّا مَنِ ٱسْتَغْنَىٰ

    Unukuzi: Amma manis taghnaa

    Ama ajionaye hana haja,

  6. 6

    فَأَنتَ لَهُۥ تَصَدَّىٰ

    Unukuzi: Fa-anta lahu tasaddaa

    Wewe ndio unamshughulikia?

  7. 7

    وَمَا عَلَيْكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ

    Unukuzi: Wa ma 'alaika allaa yaz zakka.

    Na si juu yako kama hakutakasika.

  8. 8

    وَأَمَّا مَن جَآءَكَ يَسْعَىٰ

    Unukuzi: Wa amma man jaa-aka yas'a

    Ama anaye kujia kwa juhudi,

  9. 9

    وَهُوَ يَخْشَىٰ

    Unukuzi: Wahuwa yakhshaa,

    Naye anaogopa,

  10. 10

    فَأَنتَ عَنْهُ تَلَهَّىٰ

    Unukuzi: Fa-anta 'anhu talah haa.

    Ndio wewe unampuuza?

  11. 11

    كَلَّآ إِنَّهَا تَذْكِرَةٌۭ

    Unukuzi: Kalla innaha tazkirah

    Sivyo hivyo! Huku ni kukumbushana.

  12. 12

    فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ

    Unukuzi: Faman shaa a zakarah

    Basi anaye penda akumbuke.

  13. 13

    فِى صُحُفٍۢ مُّكَرَّمَةٍۢ

    Unukuzi: Fi suhufim mukar rama,

    Yamo katika kurasa zilizo hishimiwa,

  14. 14

    مَّرْفُوعَةٍۢ مُّطَهَّرَةٍۭ

    Unukuzi: Marfoo'atim mutah hara,

    Zilizo inuliwa, zilizo takaswa.

  15. 15

    بِأَيْدِى سَفَرَةٍۢ

    Unukuzi: Bi'aidee safara

    Zimo mikononi mwa Malaika waandishi,

  16. 16

    كِرَامٍۭ بَرَرَةٍۢ

    Unukuzi: Kiraamim bararah.

    Watukufu, wema.

  17. 17

    قُتِلَ ٱلْإِنسَٰنُ مَآ أَكْفَرَهُۥ

    Unukuzi: Qutilal-insanu maa akfarah.

    Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha?

  18. 18

    مِنْ أَىِّ شَىْءٍ خَلَقَهُۥ

    Unukuzi: Min aiyyi shai-in Khalaq

    Kwa kitu gani amemuumba?

  19. 19

    مِن نُّطْفَةٍ خَلَقَهُۥ فَقَدَّرَهُۥ

    Unukuzi: Min nutfah; khalaqahu faqad-darah.

    Kwa tone la manii, akamuumba na akamkadiria.

  20. 20

    ثُمَّ ٱلسَّبِيلَ يَسَّرَهُۥ

    Unukuzi: Thummas sabeela yas-sarah

    Kisha akamsahilishia njia.

  21. 21

    ثُمَّ أَمَاتَهُۥ فَأَقْبَرَهُۥ

    Unukuzi: Thumma amatahu fa-aqbarah

    Kisha akamfisha, akamtia kaburini.

  22. 22

    ثُمَّ إِذَا شَآءَ أَنشَرَهُۥ

    Unukuzi: Thumma iza shaa-a ansharah

    Kisha apendapo atamfufua.

  23. 23

    كَلَّا لَمَّا يَقْضِ مَآ أَمَرَهُۥ

    Unukuzi: Kalla lamma yaqdi maa amarah.

    La! Hajamaliza aliyo muamuru.

  24. 24

    فَلْيَنظُرِ ٱلْإِنسَٰنُ إِلَىٰ طَعَامِهِۦٓ

    Unukuzi: Falyanzuril insanu ilaa ta-amih

    Hebu mtu na atazame chakula chake.

  25. 25

    أَنَّا صَبَبْنَا ٱلْمَآءَ صَبًّۭا

    Unukuzi: Anna sabab nalmaa-a sabba.

    Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu,

  26. 26

    ثُمَّ شَقَقْنَا ٱلْأَرْضَ شَقًّۭا

    Unukuzi: Thumma sha qaqnal-arda shaqqa.

    Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu,

  27. 27

    فَأَنۢبَتْنَا فِيهَا حَبًّۭا

    Unukuzi: Fa ambatna feeha habba

    Kisha tukaotesha humo nafaka,

  28. 28

    وَعِنَبًۭا وَقَضْبًۭا

    Unukuzi: Wa 'inabaw-wa qadba

    Na zabibu, na mimea ya majani,

  29. 29

    وَزَيْتُونًۭا وَنَخْلًۭا

    Unukuzi: Wa zaitoonaw wanakh la'

    Na mizaituni, na mitende,

  30. 30

    وَحَدَآئِقَ غُلْبًۭا

    Unukuzi: Wa hadaa-iqa ghulba

    Na bustani zenye miti iliyo songana baraabara,

  31. 31

    وَفَٰكِهَةًۭ وَأَبًّۭا

    Unukuzi: Wa faki hataw-wa abba.

    Na matunda, na malisho ya wanyama;

  32. 32

    مَّتَٰعًۭا لَّكُمْ وَلِأَنْعَٰمِكُمْ

    Unukuzi: Mata'al-lakum wa li-an'amikum.

    Kwa manufaa yenu na mifugo yenu.

  33. 33

    فَإِذَا جَآءَتِ ٱلصَّآخَّةُ

    Unukuzi: Faiza jaa-atis saakhah.

    Basi utakapo kuja ukelele,

  34. 34

    يَوْمَ يَفِرُّ ٱلْمَرْءُ مِنْ أَخِيهِ

    Unukuzi: Yauma yafir-rul mar-u min akheeh

    Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye,

  35. 35

    وَأُمِّهِۦ وَأَبِيهِ

    Unukuzi: Wa ummihee wa abeeh

    Na mamaye na babaye,

  36. 36

    وَصَٰحِبَتِهِۦ وَبَنِيهِ

    Unukuzi: Wa sahi batihee wa baneeh.

    Na mkewe na wanawe -

  37. 37

    لِكُلِّ ٱمْرِئٍۢ مِّنْهُمْ يَوْمَئِذٍۢ شَأْنٌۭ يُغْنِيهِ

    Unukuzi: Likul limri-im-minuhm yaumaa-izin shaa nuy-yughneeh

    Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha.

  38. 38

    وُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍۢ مُّسْفِرَةٌۭ

    Unukuzi: Wujoo huny-yauma-izim-musfira;

    Siku hiyo ziko nyuso zitazo nawiri,

  39. 39

    ضَاحِكَةٌۭ مُّسْتَبْشِرَةٌۭ

    Unukuzi: Dahi katum mustab shirah

    Zitacheka, zitachangamka;

  40. 40

    وَوُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍ عَلَيْهَا غَبَرَةٌۭ

    Unukuzi: Wa wujoohuy yauma-izin 'alaiha ghabar a

    Na nyuso siku hiyo zitakuwa na mavumbi,

  41. 41

    تَرْهَقُهَا قَتَرَةٌ

    Unukuzi: Tarhaquha qatarah.

    Giza totoro litazifunika,

  42. 42

    أُو۟لَٰٓئِكَ هُمُ ٱلْكَفَرَةُ ٱلْفَجَرَةُ

    Unukuzi: Ulaa-ika humul-kafa ratul-fajarah.

    Hao ndio makafiri watenda maovu.

Toleo la tafsiri: sw.barwani

Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).

Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.

Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.

He Frowned — Islam Word