Sura zote

Surah 79

Those who drag forth

سُورَةُ النَّازِعَاتِ

An-Naazi'aat · Makka

Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia

Sauti
  1. 1

    بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَٱلنَّٰزِعَٰتِ غَرْقًۭا

    Unukuzi: Wan naazi 'aati gharqa

    Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu,

  2. 2

    وَٱلنَّٰشِطَٰتِ نَشْطًۭا

    Unukuzi: Wan naa shi taati nashta

    Na kwa wanao toa kwa upole,

  3. 3

    وَٱلسَّٰبِحَٰتِ سَبْحًۭا

    Unukuzi: Wass saabi-haati sabha

    Na wanao ogelea,

  4. 4

    فَٱلسَّٰبِقَٰتِ سَبْقًۭا

    Unukuzi: Fass saabi qaati sabqa

    Wakishindana mbio,

  5. 5

    فَٱلْمُدَبِّرَٰتِ أَمْرًۭا

    Unukuzi: Fal mu dab-bi raati amra

    Wakidabiri mambo.

  6. 6

    يَوْمَ تَرْجُفُ ٱلرَّاجِفَةُ

    Unukuzi: Yawma tarjufur raajifa

    Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka,

  7. 7

    تَتْبَعُهَا ٱلرَّادِفَةُ

    Unukuzi: Tatba'u har raadifa

    Kifuate cha kufuatia.

  8. 8

    قُلُوبٌۭ يَوْمَئِذٍۢ وَاجِفَةٌ

    Unukuzi: Quloobuny-yau maaiziw-waaji-fa

    Siku hiyo nyoyo zitapiga piga,

  9. 9

    أَبْصَٰرُهَا خَٰشِعَةٌۭ

    Unukuzi: Absaa ruhaa khashi'ah

    Macho yatainama chini.

  10. 10

    يَقُولُونَ أَءِنَّا لَمَرْدُودُونَ فِى ٱلْحَافِرَةِ

    Unukuzi: Ya qoo loona a-inna lamar doo doona fil haafirah

    Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?

  11. 11

    أَءِذَا كُنَّا عِظَٰمًۭا نَّخِرَةًۭ

    Unukuzi: Aizaa kunna 'izaa man-nakhirah

    Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?

  12. 12

    قَالُوا۟ تِلْكَ إِذًۭا كَرَّةٌ خَاسِرَةٌۭ

    Unukuzi: Qaalu tilka izan karratun khaasirah.

    Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!

  13. 13

    فَإِنَّمَا هِىَ زَجْرَةٌۭ وَٰحِدَةٌۭ

    Unukuzi: Fa inna ma hiya zajratuw-waahida

    Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,

  14. 14

    فَإِذَا هُم بِٱلسَّاهِرَةِ

    Unukuzi: Faizaa hum biss saahirah

    Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!

  15. 15

    هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ

    Unukuzi: Hal ataaka hadeethu Musaa

    Je! Imekufikia hadithi ya Musa?

  16. 16

    إِذْ نَادَىٰهُ رَبُّهُۥ بِٱلْوَادِ ٱلْمُقَدَّسِ طُوًى

    Unukuzi: Iz nadaahu rabbuhu bil waadil-muqad dasi tuwa

    Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:

  17. 17

    ٱذْهَبْ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ

    Unukuzi: Izhab ilaa fir'auna innahu taghaa.

    Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri.

  18. 18

    فَقُلْ هَل لَّكَ إِلَىٰٓ أَن تَزَكَّىٰ

    Unukuzi: Faqul hal laka ilaa-an tazakka.

    Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?

  19. 19

    وَأَهْدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخْشَىٰ

    Unukuzi: Wa ahdi yaka ila rabbika fatakh sha

    Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.

  20. 20

    فَأَرَىٰهُ ٱلْءَايَةَ ٱلْكُبْرَىٰ

    Unukuzi: Fa araahul-aayatal kubra.

    Basi alimwonyesha Ishara kubwa.

  21. 21

    فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ

    Unukuzi: Fa kazzaba wa asaa.

    Lakini aliikadhibisha na akaasi.

  22. 22

    ثُمَّ أَدْبَرَ يَسْعَىٰ

    Unukuzi: Thumma adbara yas'aa.

    Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.

  23. 23

    فَحَشَرَ فَنَادَىٰ

    Unukuzi: Fa hashara fanada.

    Akakusanya watu akanadi.

  24. 24

    فَقَالَ أَنَا۠ رَبُّكُمُ ٱلْأَعْلَىٰ

    Unukuzi: Faqala ana rabbu kumul-a'laa.

    Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.

  25. 25

    فَأَخَذَهُ ٱللَّهُ نَكَالَ ٱلْءَاخِرَةِ وَٱلْأُولَىٰٓ

    Unukuzi: Fa-akha zahul laahu nakalal aakhirati wal-oola.

    Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.

  26. 26

    إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَعِبْرَةًۭ لِّمَن يَخْشَىٰٓ

    Unukuzi: Inna fee zaalika la'ibratal limaiy-yaksha

    Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.

  27. 27

    ءَأَنتُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَمِ ٱلسَّمَآءُ ۚ بَنَىٰهَا

    Unukuzi: A-antum a shaddu khalqan amis samaa-u banaaha.

    Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!

  28. 28

    رَفَعَ سَمْكَهَا فَسَوَّىٰهَا

    Unukuzi: Raf'a sam kaha fasaw waaha

    Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.

  29. 29

    وَأَغْطَشَ لَيْلَهَا وَأَخْرَجَ ضُحَىٰهَا

    Unukuzi: Wa aghtasha lailaha wa akhraja duhaaha.

    Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake.

  30. 30

    وَٱلْأَرْضَ بَعْدَ ذَٰلِكَ دَحَىٰهَآ

    Unukuzi: Wal arda b'ada zaalika dahaaha.

    Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.

  31. 31

    أَخْرَجَ مِنْهَا مَآءَهَا وَمَرْعَىٰهَا

    Unukuzi: Akhraja minha maa-aha wa mar 'aaha.

    Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake,

  32. 32

    وَٱلْجِبَالَ أَرْسَىٰهَا

    Unukuzi: Wal jibala arsaaha.

    Na milima akaisimamisha,

  33. 33

    مَتَٰعًۭا لَّكُمْ وَلِأَنْعَٰمِكُمْ

    Unukuzi: Mataa'al lakum wali an 'aamikum.

    Kwa nafuu yenu na mifugo yenu.

  34. 34

    فَإِذَا جَآءَتِ ٱلطَّآمَّةُ ٱلْكُبْرَىٰ

    Unukuzi: Fa-izaa jaaa'atit taaam matul kubraa.

    Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa,

  35. 35

    يَوْمَ يَتَذَكَّرُ ٱلْإِنسَٰنُ مَا سَعَىٰ

    Unukuzi: Yauma Yata zakkarul insaanu ma sa'aa.

    Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya,

  36. 36

    وَبُرِّزَتِ ٱلْجَحِيمُ لِمَن يَرَىٰ

    Unukuzi: Wa burrizatil-jaheemu limany-yaraa.

    Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,

  37. 37

    فَأَمَّا مَن طَغَىٰ

    Unukuzi: Fa ammaa man taghaa.

    Basi ama yule aliye zidi ujeuri,

  38. 38

    وَءَاثَرَ ٱلْحَيَوٰةَ ٱلدُّنْيَا

    Unukuzi: Wa aasaral hayaatad dunyaa

    Na akakhiari maisha ya dunia,

  39. 39

    فَإِنَّ ٱلْجَحِيمَ هِىَ ٱلْمَأْوَىٰ

    Unukuzi: Fa innal jaheema hiyal maawaa.

    Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!

  40. 40

    وَأَمَّا مَنْ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ وَنَهَى ٱلنَّفْسَ عَنِ ٱلْهَوَىٰ

    Unukuzi: Wa ammaa man khaafa maqaama Rabbihee wa nahan nafsa 'anil hawaa

    Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,

  41. 41

    فَإِنَّ ٱلْجَنَّةَ هِىَ ٱلْمَأْوَىٰ

    Unukuzi: Fa innal jannata hiyal maawaa

    Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!

  42. 42

    يَسْـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلسَّاعَةِ أَيَّانَ مُرْسَىٰهَا

    Unukuzi: Yas'aloonaka 'anis saa'ati ayyaana mursaahaa

    Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini?

  43. 43

    فِيمَ أَنتَ مِن ذِكْرَىٰهَآ

    Unukuzi: Feema anta min zikraahaa

    Una nini wewe hata uitaje?

  44. 44

    إِلَىٰ رَبِّكَ مُنتَهَىٰهَآ

    Unukuzi: Ilaa Rabbika muntahaa haa

    Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake.

  45. 45

    إِنَّمَآ أَنتَ مُنذِرُ مَن يَخْشَىٰهَا

    Unukuzi: Innamaaa anta munziru maiy yakshaahaa

    Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu.

  46. 46

    كَأَنَّهُمْ يَوْمَ يَرَوْنَهَا لَمْ يَلْبَثُوٓا۟ إِلَّا عَشِيَّةً أَوْ ضُحَىٰهَا

    Unukuzi: Ka annahum Yawma yarawnahaa lam yalbasooo illaa 'ashiyyatan aw duhaahaa

    Ni kama kwamba wao siku watapo iona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake.

Toleo la tafsiri: sw.barwani

Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).

Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.

Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.

Those who drag forth — Islam Word