Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia
- 1
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَٱلنَّٰزِعَٰتِ غَرْقًۭا
Unukuzi: Wan naazi 'aati gharqa
Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu,
- 2
وَٱلنَّٰشِطَٰتِ نَشْطًۭا
Unukuzi: Wan naa shi taati nashta
Na kwa wanao toa kwa upole,
- 3
وَٱلسَّٰبِحَٰتِ سَبْحًۭا
Unukuzi: Wass saabi-haati sabha
Na wanao ogelea,
- 4
فَٱلسَّٰبِقَٰتِ سَبْقًۭا
Unukuzi: Fass saabi qaati sabqa
Wakishindana mbio,
- 5
فَٱلْمُدَبِّرَٰتِ أَمْرًۭا
Unukuzi: Fal mu dab-bi raati amra
Wakidabiri mambo.
- 6
يَوْمَ تَرْجُفُ ٱلرَّاجِفَةُ
Unukuzi: Yawma tarjufur raajifa
Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka,
- 7
تَتْبَعُهَا ٱلرَّادِفَةُ
Unukuzi: Tatba'u har raadifa
Kifuate cha kufuatia.
- 8
قُلُوبٌۭ يَوْمَئِذٍۢ وَاجِفَةٌ
Unukuzi: Quloobuny-yau maaiziw-waaji-fa
Siku hiyo nyoyo zitapiga piga,
- 9
أَبْصَٰرُهَا خَٰشِعَةٌۭ
Unukuzi: Absaa ruhaa khashi'ah
Macho yatainama chini.
- 10
يَقُولُونَ أَءِنَّا لَمَرْدُودُونَ فِى ٱلْحَافِرَةِ
Unukuzi: Ya qoo loona a-inna lamar doo doona fil haafirah
Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?
- 11
أَءِذَا كُنَّا عِظَٰمًۭا نَّخِرَةًۭ
Unukuzi: Aizaa kunna 'izaa man-nakhirah
Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?
- 12
قَالُوا۟ تِلْكَ إِذًۭا كَرَّةٌ خَاسِرَةٌۭ
Unukuzi: Qaalu tilka izan karratun khaasirah.
Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!
- 13
فَإِنَّمَا هِىَ زَجْرَةٌۭ وَٰحِدَةٌۭ
Unukuzi: Fa inna ma hiya zajratuw-waahida
Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,
- 14
فَإِذَا هُم بِٱلسَّاهِرَةِ
Unukuzi: Faizaa hum biss saahirah
Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!
- 15
هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ
Unukuzi: Hal ataaka hadeethu Musaa
Je! Imekufikia hadithi ya Musa?
- 16
إِذْ نَادَىٰهُ رَبُّهُۥ بِٱلْوَادِ ٱلْمُقَدَّسِ طُوًى
Unukuzi: Iz nadaahu rabbuhu bil waadil-muqad dasi tuwa
Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:
- 17
ٱذْهَبْ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ
Unukuzi: Izhab ilaa fir'auna innahu taghaa.
Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri.
- 18
فَقُلْ هَل لَّكَ إِلَىٰٓ أَن تَزَكَّىٰ
Unukuzi: Faqul hal laka ilaa-an tazakka.
Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?
- 19
وَأَهْدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخْشَىٰ
Unukuzi: Wa ahdi yaka ila rabbika fatakh sha
Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.
- 20
فَأَرَىٰهُ ٱلْءَايَةَ ٱلْكُبْرَىٰ
Unukuzi: Fa araahul-aayatal kubra.
Basi alimwonyesha Ishara kubwa.
- 21
فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ
Unukuzi: Fa kazzaba wa asaa.
Lakini aliikadhibisha na akaasi.
- 22
ثُمَّ أَدْبَرَ يَسْعَىٰ
Unukuzi: Thumma adbara yas'aa.
Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.
- 23
فَحَشَرَ فَنَادَىٰ
Unukuzi: Fa hashara fanada.
Akakusanya watu akanadi.
- 24
فَقَالَ أَنَا۠ رَبُّكُمُ ٱلْأَعْلَىٰ
Unukuzi: Faqala ana rabbu kumul-a'laa.
Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.
- 25
فَأَخَذَهُ ٱللَّهُ نَكَالَ ٱلْءَاخِرَةِ وَٱلْأُولَىٰٓ
Unukuzi: Fa-akha zahul laahu nakalal aakhirati wal-oola.
Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.
- 26
إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَعِبْرَةًۭ لِّمَن يَخْشَىٰٓ
Unukuzi: Inna fee zaalika la'ibratal limaiy-yaksha
Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.
- 27
ءَأَنتُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَمِ ٱلسَّمَآءُ ۚ بَنَىٰهَا
Unukuzi: A-antum a shaddu khalqan amis samaa-u banaaha.
Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!
- 28
رَفَعَ سَمْكَهَا فَسَوَّىٰهَا
Unukuzi: Raf'a sam kaha fasaw waaha
Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.
- 29
وَأَغْطَشَ لَيْلَهَا وَأَخْرَجَ ضُحَىٰهَا
Unukuzi: Wa aghtasha lailaha wa akhraja duhaaha.
Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake.
- 30
وَٱلْأَرْضَ بَعْدَ ذَٰلِكَ دَحَىٰهَآ
Unukuzi: Wal arda b'ada zaalika dahaaha.
Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.
- 31
أَخْرَجَ مِنْهَا مَآءَهَا وَمَرْعَىٰهَا
Unukuzi: Akhraja minha maa-aha wa mar 'aaha.
Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake,
- 32
وَٱلْجِبَالَ أَرْسَىٰهَا
Unukuzi: Wal jibala arsaaha.
Na milima akaisimamisha,
- 33
مَتَٰعًۭا لَّكُمْ وَلِأَنْعَٰمِكُمْ
Unukuzi: Mataa'al lakum wali an 'aamikum.
Kwa nafuu yenu na mifugo yenu.
- 34
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلطَّآمَّةُ ٱلْكُبْرَىٰ
Unukuzi: Fa-izaa jaaa'atit taaam matul kubraa.
Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa,
- 35
يَوْمَ يَتَذَكَّرُ ٱلْإِنسَٰنُ مَا سَعَىٰ
Unukuzi: Yauma Yata zakkarul insaanu ma sa'aa.
Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya,
- 36
وَبُرِّزَتِ ٱلْجَحِيمُ لِمَن يَرَىٰ
Unukuzi: Wa burrizatil-jaheemu limany-yaraa.
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,
- 37
فَأَمَّا مَن طَغَىٰ
Unukuzi: Fa ammaa man taghaa.
Basi ama yule aliye zidi ujeuri,
- 38
وَءَاثَرَ ٱلْحَيَوٰةَ ٱلدُّنْيَا
Unukuzi: Wa aasaral hayaatad dunyaa
Na akakhiari maisha ya dunia,
- 39
فَإِنَّ ٱلْجَحِيمَ هِىَ ٱلْمَأْوَىٰ
Unukuzi: Fa innal jaheema hiyal maawaa.
Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!
- 40
وَأَمَّا مَنْ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ وَنَهَى ٱلنَّفْسَ عَنِ ٱلْهَوَىٰ
Unukuzi: Wa ammaa man khaafa maqaama Rabbihee wa nahan nafsa 'anil hawaa
Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,
- 41
فَإِنَّ ٱلْجَنَّةَ هِىَ ٱلْمَأْوَىٰ
Unukuzi: Fa innal jannata hiyal maawaa
Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!
- 42
يَسْـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلسَّاعَةِ أَيَّانَ مُرْسَىٰهَا
Unukuzi: Yas'aloonaka 'anis saa'ati ayyaana mursaahaa
Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini?
- 43
فِيمَ أَنتَ مِن ذِكْرَىٰهَآ
Unukuzi: Feema anta min zikraahaa
Una nini wewe hata uitaje?
- 44
إِلَىٰ رَبِّكَ مُنتَهَىٰهَآ
Unukuzi: Ilaa Rabbika muntahaa haa
Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake.
- 45
إِنَّمَآ أَنتَ مُنذِرُ مَن يَخْشَىٰهَا
Unukuzi: Innamaaa anta munziru maiy yakshaahaa
Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu.
- 46
كَأَنَّهُمْ يَوْمَ يَرَوْنَهَا لَمْ يَلْبَثُوٓا۟ إِلَّا عَشِيَّةً أَوْ ضُحَىٰهَا
Unukuzi: Ka annahum Yawma yarawnahaa lam yalbasooo illaa 'ashiyyatan aw duhaahaa
Ni kama kwamba wao siku watapo iona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake.
Toleo la tafsiri: sw.barwani
Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).
Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.
Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.