Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia
- 1
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ عَمَّ يَتَسَآءَلُونَ
Unukuzi: 'Amma Yatasaa-aloon
WANAULIZANA nini?
- 2
عَنِ ٱلنَّبَإِ ٱلْعَظِيمِ
Unukuzi: 'Anin-nabaa-il 'azeem
Ile khabari kuu,
- 3
ٱلَّذِى هُمْ فِيهِ مُخْتَلِفُونَ
Unukuzi: Allazi hum feehi mukh talifoon
Ambayo kwayo wanakhitalifiana.
- 4
كَلَّا سَيَعْلَمُونَ
Unukuzi: Kallaa sa y'alamoon
La! Karibu watakuja jua.
- 5
ثُمَّ كَلَّا سَيَعْلَمُونَ
Unukuzi: Thumma kallaa sa y'alamoon
Tena la! Karibu watakuja jua.
- 6
أَلَمْ نَجْعَلِ ٱلْأَرْضَ مِهَٰدًۭا
Unukuzi: Alam naj'alil arda mihaa da
Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko?
- 7
وَٱلْجِبَالَ أَوْتَادًۭا
Unukuzi: Wal jibaala au taada
Na milima kama vigingi?
- 8
وَخَلَقْنَٰكُمْ أَزْوَٰجًۭا
Unukuzi: Wa khalaq naakum azwaaja
Na tukakuumbeni kwa jozi?
- 9
وَجَعَلْنَا نَوْمَكُمْ سُبَاتًۭا
Unukuzi: Waja'alnan naumakum subata
Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko?
- 10
وَجَعَلْنَا ٱلَّيْلَ لِبَاسًۭا
Unukuzi: Waja'alnal laila libasa
Na tukaufanya usiku ni nguo?
- 11
وَجَعَلْنَا ٱلنَّهَارَ مَعَاشًۭا
Unukuzi: Waja'alnan nahara ma 'aasha
Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha?
- 12
وَبَنَيْنَا فَوْقَكُمْ سَبْعًۭا شِدَادًۭا
Unukuzi: Wa banaina fauqakum sab 'an shi daada
Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?
- 13
وَجَعَلْنَا سِرَاجًۭا وَهَّاجًۭا
Unukuzi: Waja'alna siraajaw wah haaja
Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto;
- 14
وَأَنزَلْنَا مِنَ ٱلْمُعْصِرَٰتِ مَآءًۭ ثَجَّاجًۭا
Unukuzi: Wa anzalna minal m'usiraati maa-an saj-jaaja
Na tukateremsha maji yanayo anguka kwa kasi kutoka mawinguni,
- 15
لِّنُخْرِجَ بِهِۦ حَبًّۭا وَنَبَاتًۭا
Unukuzi: Linukh rija bihee habbaw wana baata
Ili tutoe kwayo nafaka na mimea,
- 16
وَجَنَّٰتٍ أَلْفَافًا
Unukuzi: Wa jan naatin alfafa
Na mabustani yenye miti iliyo kamatana.
- 17
إِنَّ يَوْمَ ٱلْفَصْلِ كَانَ مِيقَٰتًۭا
Unukuzi: Inna yaumal-fasli kana miqaata
Hakika siku ya uamuzi imewekewa wakati wake,
- 18
يَوْمَ يُنفَخُ فِى ٱلصُّورِ فَتَأْتُونَ أَفْوَاجًۭا
Unukuzi: Yauma yun fakhu fis-soori fataa toona afwaaja
Siku litapo pulizwa barugumu, nanyi mtakuja kwa makundi,
- 19
وَفُتِحَتِ ٱلسَّمَآءُ فَكَانَتْ أَبْوَٰبًۭا
Unukuzi: Wa futiha tis samaa-u fakaanat abwaaba
Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango,
- 20
وَسُيِّرَتِ ٱلْجِبَالُ فَكَانَتْ سَرَابًا
Unukuzi: Wa suyyi raatil jibaalu fa kaanat saraaba
Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.
- 21
إِنَّ جَهَنَّمَ كَانَتْ مِرْصَادًۭا
Unukuzi: Inna jahan nama kaanat mirsaada
Hakika Jahannamu inangojea!
- 22
لِّلطَّٰغِينَ مَـَٔابًۭا
Unukuzi: Lit taa gheena ma aaba
Kwa walio asi ndio makaazi yao,
- 23
لَّٰبِثِينَ فِيهَآ أَحْقَابًۭا
Unukuzi: Laa bitheena feehaa ahqaaba
Wakae humo karne baada ya karne,
- 24
لَّا يَذُوقُونَ فِيهَا بَرْدًۭا وَلَا شَرَابًا
Unukuzi: Laa ya zooqoona feeha bar daw walaa sharaaba
Hawataonja humo chochote kibaridi wala kinywaji,
- 25
إِلَّا حَمِيمًۭا وَغَسَّاقًۭا
Unukuzi: Illa hamee maw-wa ghas saaqa
Ila maji yamoto sana na usaha,
- 26
جَزَآءًۭ وِفَاقًا
Unukuzi: Jazaa-aw wi faaqa
Ndio jaza muwafaka.
- 27
إِنَّهُمْ كَانُوا۟ لَا يَرْجُونَ حِسَابًۭا
Unukuzi: Innahum kaanu laa yarjoona hisaaba
Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hisabu.
- 28
وَكَذَّبُوا۟ بِـَٔايَٰتِنَا كِذَّابًۭا
Unukuzi: Wa kazzabu bi aayaa tina kizzaba
Na wakikanusha Aya zetu kwa nguvu.
- 29
وَكُلَّ شَىْءٍ أَحْصَيْنَٰهُ كِتَٰبًۭا
Unukuzi: Wa kulla shai-in ahsai naahu kitaa ba
Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika.
- 30
فَذُوقُوا۟ فَلَن نَّزِيدَكُمْ إِلَّا عَذَابًا
Unukuzi: Fa zooqoo falan-nazee dakum ill-laa azaaba
Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!
- 31
إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ مَفَازًا
Unukuzi: Inna lil mutta qeena mafaaza
Hakika wachamngu wanastahiki kufuzu,
- 32
حَدَآئِقَ وَأَعْنَٰبًۭا
Unukuzi: Hadaa-iqa wa a'anaa ba
Mabustani na mizabibu,
- 33
وَكَوَاعِبَ أَتْرَابًۭا
Unukuzi: Wa kaawa 'iba at raaba
Na wake walio lingana nao,
- 34
وَكَأْسًۭا دِهَاقًۭا
Unukuzi: Wa ka'san di haaqa
Na bilauri zilizo jaa,
- 35
لَّا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًۭا وَلَا كِذَّٰبًۭا
Unukuzi: Laa yasma'oona fiha lagh waw walaa kizzaba
Hawatasikia humo upuuzi wala uwongo -
- 36
جَزَآءًۭ مِّن رَّبِّكَ عَطَآءً حِسَابًۭا
Unukuzi: Jazaa-am mir-rabbika ataa-an hisaaba
Malipo kutoka kwa Mola wako Mlezi, kipawa cha kutosha.
- 37
رَّبِّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا ٱلرَّحْمَٰنِ ۖ لَا يَمْلِكُونَ مِنْهُ خِطَابًۭا
Unukuzi: Rabbis samaa waati wal ardi wa maa baina humar rahmaani laa yam likoona minhu khi taaba
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, Arrahman, Mwingi wa rehema; hawamiliki usemi mbele yake!
- 38
يَوْمَ يَقُومُ ٱلرُّوحُ وَٱلْمَلَٰٓئِكَةُ صَفًّۭا ۖ لَّا يَتَكَلَّمُونَ إِلَّا مَنْ أَذِنَ لَهُ ٱلرَّحْمَٰنُ وَقَالَ صَوَابًۭا
Unukuzi: Yauma yaqoo mur roohu wal malaa-ikatu saf-fal laa yata kalla moona illa man azina lahur rahmaanu wa qaala sawaaba
Siku atakapo simama Roho na Malaika kwa safu. Hawatasema ila Mwingi wa rehema aliye mruhusu, na atasema yaliyo sawa tu.
- 39
ذَٰلِكَ ٱلْيَوْمُ ٱلْحَقُّ ۖ فَمَن شَآءَ ٱتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِۦ مَـَٔابًا
Unukuzi: Zaalikal yaumul haqqu faman shaa-at ta khaaza ill-laa rabbihi ma-aaba
Hiyo ndiyo Siku ya haki. Basi anaye taka na ashike njia arejee kwa Mola wake Mlezi.
- 40
إِنَّآ أَنذَرْنَٰكُمْ عَذَابًۭا قَرِيبًۭا يَوْمَ يَنظُرُ ٱلْمَرْءُ مَا قَدَّمَتْ يَدَاهُ وَيَقُولُ ٱلْكَافِرُ يَٰلَيْتَنِى كُنتُ تُرَٰبًۢا
Unukuzi: In naa anzar naakum azaaban qareebaiy-yauma yan zurul marr-u maa qaddamat yadaahu wa ya qoolul-kaafiru yaa lai tanee kuntu turaaba
Hakika tumekuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika; Siku ambayo mtu atakapo ona yaliyo tangulizwa na mikono yake; na kafiri atasema: Laiti ningeli kuwa udongo!
Toleo la tafsiri: sw.barwani
Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).
Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.
Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.