Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia
- 1
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَٱلْعَٰدِيَٰتِ ضَبْحًۭا
Unukuzi: Wal'aadi yaati dabha
Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua,
- 2
فَٱلْمُورِيَٰتِ قَدْحًۭا
Unukuzi: Fal moori yaati qadha
Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini,
- 3
فَٱلْمُغِيرَٰتِ صُبْحًۭا
Unukuzi: Fal mugheeraati subha
Wakishambulia wakati wa asubuhi,
- 4
فَأَثَرْنَ بِهِۦ نَقْعًۭا
Unukuzi: Fa atharna bihee naq'a
Huku wakitimua vumbi,
- 5
فَوَسَطْنَ بِهِۦ جَمْعًا
Unukuzi: Fawa satna bihee jam'a
Na wakijitoma kati ya kundi,
- 6
إِنَّ ٱلْإِنسَٰنَ لِرَبِّهِۦ لَكَنُودٌۭ
Unukuzi: Innal-insana lirabbihee lakanood
Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi!
- 7
وَإِنَّهُۥ عَلَىٰ ذَٰلِكَ لَشَهِيدٌۭ
Unukuzi: Wa innahu 'alaa zaalika la shaheed
Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo!
- 8
وَإِنَّهُۥ لِحُبِّ ٱلْخَيْرِ لَشَدِيدٌ
Unukuzi: Wa innahu lihubbil khairi la shadeed
Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali!
- 9
۞ أَفَلَا يَعْلَمُ إِذَا بُعْثِرَ مَا فِى ٱلْقُبُورِ
Unukuzi: Afala ya'lamu iza b'uthira ma filquboor
Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini?
- 10
وَحُصِّلَ مَا فِى ٱلصُّدُورِ
Unukuzi: Wa hussila maa fis sudoor
Na yakakusanywa yaliomo vifuani?
- 11
إِنَّ رَبَّهُم بِهِمْ يَوْمَئِذٍۢ لَّخَبِيرٌۢ
Unukuzi: Inna rabbahum bihim yauma 'izil la khabeer
Kuwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote!
Toleo la tafsiri: sw.barwani
Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).
Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.
Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.