Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia
- 1
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ ٱلْقَارِعَةُ
Unukuzi: Al qaari'ah
Inayo gonga!
- 2
مَا ٱلْقَارِعَةُ
Unukuzi: Mal qaariah
Nini Inayo gonga?
- 3
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلْقَارِعَةُ
Unukuzi: Wa maa adraaka mal qaari'ah
Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga?
- 4
يَوْمَ يَكُونُ ٱلنَّاسُ كَٱلْفَرَاشِ ٱلْمَبْثُوثِ
Unukuzi: Yauma ya koonun naasu kal farashil mabthooth
Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika;
- 5
وَتَكُونُ ٱلْجِبَالُ كَٱلْعِهْنِ ٱلْمَنفُوشِ
Unukuzi: Wa ta koonul jibalu kal 'ihnil manfoosh
Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa!
- 6
فَأَمَّا مَن ثَقُلَتْ مَوَٰزِينُهُۥ
Unukuzi: Fa-amma man thaqulat mawa zeenuh
Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito,
- 7
فَهُوَ فِى عِيشَةٍۢ رَّاضِيَةٍۢ
Unukuzi: Fahuwa fee 'ishatir raadiyah
Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza.
- 8
وَأَمَّا مَنْ خَفَّتْ مَوَٰزِينُهُۥ
Unukuzi: Wa amma man khaffat mawa zeenuh
Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,
- 9
فَأُمُّهُۥ هَاوِيَةٌۭ
Unukuzi: Fa-ummuhu haawiyah
Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!
- 10
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا هِيَهْ
Unukuzi: Wa maa adraaka maa hiyah
Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo?
- 11
نَارٌ حَامِيَةٌۢ
Unukuzi: Naarun hamiyah
Ni Moto mkali!
Toleo la tafsiri: sw.barwani
Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).
Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.
Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.