Sura zote

Surah 75

The Resurrection

سُورَةُ القِيَامَةِ

Al-Qiyaama · Makka

Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia

Sauti
  1. 1

    بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ لَآ أُقْسِمُ بِيَوْمِ ٱلْقِيَٰمَةِ

    Unukuzi: Laaa uqsimu bi yawmil qiyaamah

    Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!

  2. 2

    وَلَآ أُقْسِمُ بِٱلنَّفْسِ ٱللَّوَّامَةِ

    Unukuzi: Wa laaa uqsimu bin nafsil lawwaamah

    Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!

  3. 3

    أَيَحْسَبُ ٱلْإِنسَٰنُ أَلَّن نَّجْمَعَ عِظَامَهُۥ

    Unukuzi: Ayahsabul insaanu al lan najm'a 'izaamah

    Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?

  4. 4

    بَلَىٰ قَٰدِرِينَ عَلَىٰٓ أَن نُّسَوِّىَ بَنَانَهُۥ

    Unukuzi: Balaa qaadireena 'alaaa an nusawwiya banaanah

    Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!

  5. 5

    بَلْ يُرِيدُ ٱلْإِنسَٰنُ لِيَفْجُرَ أَمَامَهُۥ

    Unukuzi: Bal yureedul insaanu liyafjura amaamah

    Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.

  6. 6

    يَسْـَٔلُ أَيَّانَ يَوْمُ ٱلْقِيَٰمَةِ

    Unukuzi: Yas'alu ayyyaana yawmul qiyaamah

    Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?

  7. 7

    فَإِذَا بَرِقَ ٱلْبَصَرُ

    Unukuzi: Fa izaa bariqal basar

    Basi jicho litapo dawaa,

  8. 8

    وَخَسَفَ ٱلْقَمَرُ

    Unukuzi: We khasafal qamar

    Na mwezi utapo patwa,

  9. 9

    وَجُمِعَ ٱلشَّمْسُ وَٱلْقَمَرُ

    Unukuzi: Wa jumi'ash shamusu wal qamar

    Na likakusanywa jua na mwezi,

  10. 10

    يَقُولُ ٱلْإِنسَٰنُ يَوْمَئِذٍ أَيْنَ ٱلْمَفَرُّ

    Unukuzi: Yaqoolul insaanu yaw ma 'izin aynal mafarr

    Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?

  11. 11

    كَلَّا لَا وَزَرَ

    Unukuzi: Kallaa laa wazar

    La! Hapana pa kukimbilia!

  12. 12

    إِلَىٰ رَبِّكَ يَوْمَئِذٍ ٱلْمُسْتَقَرُّ

    Unukuzi: Ilaa rabbika yawma 'izinil mustaqarr

    Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.

  13. 13

    يُنَبَّؤُا۟ ٱلْإِنسَٰنُ يَوْمَئِذٍۭ بِمَا قَدَّمَ وَأَخَّرَ

    Unukuzi: Yunabba 'ul insaanu yawma 'izim bimaa qaddama wa akhkhar

    Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.

  14. 14

    بَلِ ٱلْإِنسَٰنُ عَلَىٰ نَفْسِهِۦ بَصِيرَةٌۭ

    Unukuzi: Balil insaanu 'alaa nafsihee baseerah

    Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.

  15. 15

    وَلَوْ أَلْقَىٰ مَعَاذِيرَهُۥ

    Unukuzi: Wa law alqaa ma'aazeerah

    Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.

  16. 16

    لَا تُحَرِّكْ بِهِۦ لِسَانَكَ لِتَعْجَلَ بِهِۦٓ

    Unukuzi: Laa tuharrik bihee lisaa naka lita'jala bih

    Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.

  17. 17

    إِنَّ عَلَيْنَا جَمْعَهُۥ وَقُرْءَانَهُۥ

    Unukuzi: Inna 'alainaa jam'ahoo wa qur aanah

    Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.

  18. 18

    فَإِذَا قَرَأْنَٰهُ فَٱتَّبِعْ قُرْءَانَهُۥ

    Unukuzi: Fa izaa qaraanaahu fattabi' qur aanah

    Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.

  19. 19

    ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا بَيَانَهُۥ

    Unukuzi: Summa inna 'alainaa bayaanah

    Kisha ni juu yetu kuubainisha.

  20. 20

    كَلَّا بَلْ تُحِبُّونَ ٱلْعَاجِلَةَ

    Unukuzi: Kallaa bal tuhibboonal 'aajilah

    Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,

  21. 21

    وَتَذَرُونَ ٱلْءَاخِرَةَ

    Unukuzi: Wa tazaroonal Aakhirah

    Na mnaacha maisha ya Akhera.

  22. 22

    وُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍۢ نَّاضِرَةٌ

    Unukuzi: Wujoohuny yawma 'izin naadirah

    Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara,

  23. 23

    إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٌۭ

    Unukuzi: Ilaa rabbihaa naazirah

    Zinamwangallia Mola wao Mlezi.

  24. 24

    وَوُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍۭ بَاسِرَةٌۭ

    Unukuzi: Wa wujoohuny yawma 'izim baasirah

    Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.

  25. 25

    تَظُنُّ أَن يُفْعَلَ بِهَا فَاقِرَةٌۭ

    Unukuzi: Tazunnu any yuf'ala bihaa faaqirah

    Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.

  26. 26

    كَلَّآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلتَّرَاقِىَ

    Unukuzi: Kallaaa izaa balaghatit taraaqee

    La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,

  27. 27

    وَقِيلَ مَنْ ۜ رَاقٍۢ

    Unukuzi: Wa qeela man raaq

    Na pakasemwa: Nani wa kumganga?

  28. 28

    وَظَنَّ أَنَّهُ ٱلْفِرَاقُ

    Unukuzi: Wa zanna annahul firaaq

    Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;

  29. 29

    وَٱلْتَفَّتِ ٱلسَّاقُ بِٱلسَّاقِ

    Unukuzi: Waltaffatis saaqu bissaaq

    Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,

  30. 30

    إِلَىٰ رَبِّكَ يَوْمَئِذٍ ٱلْمَسَاقُ

    Unukuzi: Ilaa rabbika yawma'izinil masaaq

    Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!

  31. 31

    فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّىٰ

    Unukuzi: Falaa saddaqa wa laa sallaa

    Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali.

  32. 32

    وَلَٰكِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ

    Unukuzi: Wa laakin kazzaba wa tawalla

    Bali alikanusha, na akageuka.

  33. 33

    ثُمَّ ذَهَبَ إِلَىٰٓ أَهْلِهِۦ يَتَمَطَّىٰٓ

    Unukuzi: Summa zahaba ilaaa ahlihee yatamatta

    Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.

  34. 34

    أَوْلَىٰ لَكَ فَأَوْلَىٰ

    Unukuzi: Awlaa laka fa awlaa

    Ole wako, ole wako!

  35. 35

    ثُمَّ أَوْلَىٰ لَكَ فَأَوْلَىٰٓ

    Unukuzi: Summa awlaa laka fa awla

    Kisha Ole wako, ole wako!

  36. 36

    أَيَحْسَبُ ٱلْإِنسَٰنُ أَن يُتْرَكَ سُدًى

    Unukuzi: Ayahsabul insaanu anyytraka sudaa

    Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?

  37. 37

    أَلَمْ يَكُ نُطْفَةًۭ مِّن مَّنِىٍّۢ يُمْنَىٰ

    Unukuzi: Alam yaku nutfatam mim maniyyiny yumnaa

    Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?

  38. 38

    ثُمَّ كَانَ عَلَقَةًۭ فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ

    Unukuzi: Summa kaana 'alaqata fakhalaq fasawwaa

    Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.

  39. 39

    فَجَعَلَ مِنْهُ ٱلزَّوْجَيْنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلْأُنثَىٰٓ

    Unukuzi: Faja'ala minhuz zawjayniz zakara wal unsaa

    Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.

  40. 40

    أَلَيْسَ ذَٰلِكَ بِقَٰدِرٍ عَلَىٰٓ أَن يُحْۦِىَ ٱلْمَوْتَىٰ

    Unukuzi: Alaisa zaalika biqaadirin 'alaaa any yuhyiyal mawtaa

    Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?

Toleo la tafsiri: sw.barwani

Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).

Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.

Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.

The Resurrection — Islam Word