Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia
- 1
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ لَآ أُقْسِمُ بِيَوْمِ ٱلْقِيَٰمَةِ
Unukuzi: Laaa uqsimu bi yawmil qiyaamah
Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!
- 2
وَلَآ أُقْسِمُ بِٱلنَّفْسِ ٱللَّوَّامَةِ
Unukuzi: Wa laaa uqsimu bin nafsil lawwaamah
Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!
- 3
أَيَحْسَبُ ٱلْإِنسَٰنُ أَلَّن نَّجْمَعَ عِظَامَهُۥ
Unukuzi: Ayahsabul insaanu al lan najm'a 'izaamah
Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?
- 4
بَلَىٰ قَٰدِرِينَ عَلَىٰٓ أَن نُّسَوِّىَ بَنَانَهُۥ
Unukuzi: Balaa qaadireena 'alaaa an nusawwiya banaanah
Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!
- 5
بَلْ يُرِيدُ ٱلْإِنسَٰنُ لِيَفْجُرَ أَمَامَهُۥ
Unukuzi: Bal yureedul insaanu liyafjura amaamah
Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.
- 6
يَسْـَٔلُ أَيَّانَ يَوْمُ ٱلْقِيَٰمَةِ
Unukuzi: Yas'alu ayyyaana yawmul qiyaamah
Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?
- 7
فَإِذَا بَرِقَ ٱلْبَصَرُ
Unukuzi: Fa izaa bariqal basar
Basi jicho litapo dawaa,
- 8
وَخَسَفَ ٱلْقَمَرُ
Unukuzi: We khasafal qamar
Na mwezi utapo patwa,
- 9
وَجُمِعَ ٱلشَّمْسُ وَٱلْقَمَرُ
Unukuzi: Wa jumi'ash shamusu wal qamar
Na likakusanywa jua na mwezi,
- 10
يَقُولُ ٱلْإِنسَٰنُ يَوْمَئِذٍ أَيْنَ ٱلْمَفَرُّ
Unukuzi: Yaqoolul insaanu yaw ma 'izin aynal mafarr
Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?
- 11
كَلَّا لَا وَزَرَ
Unukuzi: Kallaa laa wazar
La! Hapana pa kukimbilia!
- 12
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوْمَئِذٍ ٱلْمُسْتَقَرُّ
Unukuzi: Ilaa rabbika yawma 'izinil mustaqarr
Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.
- 13
يُنَبَّؤُا۟ ٱلْإِنسَٰنُ يَوْمَئِذٍۭ بِمَا قَدَّمَ وَأَخَّرَ
Unukuzi: Yunabba 'ul insaanu yawma 'izim bimaa qaddama wa akhkhar
Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.
- 14
بَلِ ٱلْإِنسَٰنُ عَلَىٰ نَفْسِهِۦ بَصِيرَةٌۭ
Unukuzi: Balil insaanu 'alaa nafsihee baseerah
Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.
- 15
وَلَوْ أَلْقَىٰ مَعَاذِيرَهُۥ
Unukuzi: Wa law alqaa ma'aazeerah
Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.
- 16
لَا تُحَرِّكْ بِهِۦ لِسَانَكَ لِتَعْجَلَ بِهِۦٓ
Unukuzi: Laa tuharrik bihee lisaa naka lita'jala bih
Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.
- 17
إِنَّ عَلَيْنَا جَمْعَهُۥ وَقُرْءَانَهُۥ
Unukuzi: Inna 'alainaa jam'ahoo wa qur aanah
Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.
- 18
فَإِذَا قَرَأْنَٰهُ فَٱتَّبِعْ قُرْءَانَهُۥ
Unukuzi: Fa izaa qaraanaahu fattabi' qur aanah
Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.
- 19
ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا بَيَانَهُۥ
Unukuzi: Summa inna 'alainaa bayaanah
Kisha ni juu yetu kuubainisha.
- 20
كَلَّا بَلْ تُحِبُّونَ ٱلْعَاجِلَةَ
Unukuzi: Kallaa bal tuhibboonal 'aajilah
Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,
- 21
وَتَذَرُونَ ٱلْءَاخِرَةَ
Unukuzi: Wa tazaroonal Aakhirah
Na mnaacha maisha ya Akhera.
- 22
وُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍۢ نَّاضِرَةٌ
Unukuzi: Wujoohuny yawma 'izin naadirah
Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara,
- 23
إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٌۭ
Unukuzi: Ilaa rabbihaa naazirah
Zinamwangallia Mola wao Mlezi.
- 24
وَوُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍۭ بَاسِرَةٌۭ
Unukuzi: Wa wujoohuny yawma 'izim baasirah
Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.
- 25
تَظُنُّ أَن يُفْعَلَ بِهَا فَاقِرَةٌۭ
Unukuzi: Tazunnu any yuf'ala bihaa faaqirah
Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.
- 26
كَلَّآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلتَّرَاقِىَ
Unukuzi: Kallaaa izaa balaghatit taraaqee
La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,
- 27
وَقِيلَ مَنْ ۜ رَاقٍۢ
Unukuzi: Wa qeela man raaq
Na pakasemwa: Nani wa kumganga?
- 28
وَظَنَّ أَنَّهُ ٱلْفِرَاقُ
Unukuzi: Wa zanna annahul firaaq
Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;
- 29
وَٱلْتَفَّتِ ٱلسَّاقُ بِٱلسَّاقِ
Unukuzi: Waltaffatis saaqu bissaaq
Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,
- 30
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوْمَئِذٍ ٱلْمَسَاقُ
Unukuzi: Ilaa rabbika yawma'izinil masaaq
Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!
- 31
فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّىٰ
Unukuzi: Falaa saddaqa wa laa sallaa
Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali.
- 32
وَلَٰكِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ
Unukuzi: Wa laakin kazzaba wa tawalla
Bali alikanusha, na akageuka.
- 33
ثُمَّ ذَهَبَ إِلَىٰٓ أَهْلِهِۦ يَتَمَطَّىٰٓ
Unukuzi: Summa zahaba ilaaa ahlihee yatamatta
Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.
- 34
أَوْلَىٰ لَكَ فَأَوْلَىٰ
Unukuzi: Awlaa laka fa awlaa
Ole wako, ole wako!
- 35
ثُمَّ أَوْلَىٰ لَكَ فَأَوْلَىٰٓ
Unukuzi: Summa awlaa laka fa awla
Kisha Ole wako, ole wako!
- 36
أَيَحْسَبُ ٱلْإِنسَٰنُ أَن يُتْرَكَ سُدًى
Unukuzi: Ayahsabul insaanu anyytraka sudaa
Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?
- 37
أَلَمْ يَكُ نُطْفَةًۭ مِّن مَّنِىٍّۢ يُمْنَىٰ
Unukuzi: Alam yaku nutfatam mim maniyyiny yumnaa
Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?
- 38
ثُمَّ كَانَ عَلَقَةًۭ فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ
Unukuzi: Summa kaana 'alaqata fakhalaq fasawwaa
Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.
- 39
فَجَعَلَ مِنْهُ ٱلزَّوْجَيْنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلْأُنثَىٰٓ
Unukuzi: Faja'ala minhuz zawjayniz zakara wal unsaa
Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.
- 40
أَلَيْسَ ذَٰلِكَ بِقَٰدِرٍ عَلَىٰٓ أَن يُحْۦِىَ ٱلْمَوْتَىٰ
Unukuzi: Alaisa zaalika biqaadirin 'alaaa any yuhyiyal mawtaa
Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?
Toleo la tafsiri: sw.barwani
Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).
Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.
Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.