Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia
- 1
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ سَأَلَ سَآئِلٌۢ بِعَذَابٍۢ وَاقِعٍۢ
Unukuzi: Sa ala saaa'ilum bi'azaa binw-waaqi'
Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea,
- 2
لِّلْكَٰفِرِينَ لَيْسَ لَهُۥ دَافِعٌۭ
Unukuzi: Lilkaafireen laisa lahoo daafi'
Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia -
- 3
مِّنَ ٱللَّهِ ذِى ٱلْمَعَارِجِ
Unukuzi: Minal laahi zil ma'aarij
Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.
- 4
تَعْرُجُ ٱلْمَلَٰٓئِكَةُ وَٱلرُّوحُ إِلَيْهِ فِى يَوْمٍۢ كَانَ مِقْدَارُهُۥ خَمْسِينَ أَلْفَ سَنَةٍۢ
Unukuzi: Ta'rujul malaaa'ikatu war Roohu ilaihi fee yawmin kaana miqdaaruhoo khamseena alfa sanah
Malaika na Roho hupanda kwendea kwake katika siku ambayo kadiri yake ni miaka khamsini elfu!
- 5
فَٱصْبِرْ صَبْرًۭا جَمِيلًا
Unukuzi: Fasbir ssabran jameelaa
Basi subiri kwa subira njema.
- 6
إِنَّهُمْ يَرَوْنَهُۥ بَعِيدًۭا
Unukuzi: Inaahum yarawnahoo ba'eedaa
Hakika wao wanaiona iko mbali,
- 7
وَنَرَىٰهُ قَرِيبًۭا
Unukuzi: Wa naraahu qareebaa
Na Sisi tunaiona iko karibu.
- 8
يَوْمَ تَكُونُ ٱلسَّمَآءُ كَٱلْمُهْلِ
Unukuzi: Yawma takoonus samaaa'u kalmuhl
Siku ambayo mbingu zitakapo kuwa kama maadeni iliyo yayushwa.
- 9
وَتَكُونُ ٱلْجِبَالُ كَٱلْعِهْنِ
Unukuzi: Wa takoonul jibaalu kal'ihn
Na milima itakuwa kama sufi.
- 10
وَلَا يَسْـَٔلُ حَمِيمٌ حَمِيمًۭا
Unukuzi: Wa laa yas'alu hameemun hameemaa
Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake.
- 11
يُبَصَّرُونَهُمْ ۚ يَوَدُّ ٱلْمُجْرِمُ لَوْ يَفْتَدِى مِنْ عَذَابِ يَوْمِئِذٍۭ بِبَنِيهِ
Unukuzi: Yubassaroonahum; ya waddul mujrimu law yaftadee min 'azaabi yawma'izim bibaneeh
Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe,
- 12
وَصَٰحِبَتِهِۦ وَأَخِيهِ
Unukuzi: Wa saahibatihee wa akheeh
Na mkewe, na nduguye,
- 13
وَفَصِيلَتِهِ ٱلَّتِى تُـْٔوِيهِ
Unukuzi: Wa faseelathil latee tu'weeh
Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu,
- 14
وَمَن فِى ٱلْأَرْضِ جَمِيعًۭا ثُمَّ يُنجِيهِ
Unukuzi: Wa man fil ardi jamee'an summa yunjeeh
Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.
- 15
كَلَّآ ۖ إِنَّهَا لَظَىٰ
Unukuzi: Kallaa innahaa lazaa
La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,
- 16
نَزَّاعَةًۭ لِّلشَّوَىٰ
Unukuzi: Nazzaa'atal lishshawaa
Unao babua ngozi ya kichwa!
- 17
تَدْعُوا۟ مَنْ أَدْبَرَ وَتَوَلَّىٰ
Unukuzi: Tad'oo man adbara wa tawallaa
Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka.
- 18
وَجَمَعَ فَأَوْعَىٰٓ
Unukuzi: W jama'a fa aw'aa
Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi.
- 19
۞ إِنَّ ٱلْإِنسَٰنَ خُلِقَ هَلُوعًا
Unukuzi: Innal insaana khuliqa haloo'aa
Hakika mtu ameumbwa na papara.
- 20
إِذَا مَسَّهُ ٱلشَّرُّ جَزُوعًۭا
Unukuzi: Izaa massahush sharru jazoo'aa
Inapo mgusa shari hupapatika.
- 21
وَإِذَا مَسَّهُ ٱلْخَيْرُ مَنُوعًا
Unukuzi: Wa izaa massahul khairu manoo'aa
Na inapo mgusa kheri huizuilia.
- 22
إِلَّا ٱلْمُصَلِّينَ
Unukuzi: Illal musalleen
Isipo kuwa wanao sali,
- 23
ٱلَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ دَآئِمُونَ
Unukuzi: Allazeena hum 'alaa Salaatihim daaa'imoon
Ambao wanadumisha Sala zao,
- 24
وَٱلَّذِينَ فِىٓ أَمْوَٰلِهِمْ حَقٌّۭ مَّعْلُومٌۭ
Unukuzi: Wallazeena feee amwaalihim haqqum ma'loom
Na ambao katika mali yao iko haki maalumu
- 25
لِّلسَّآئِلِ وَٱلْمَحْرُومِ
Unukuzi: Lissaaa 'ili walmahroom
Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba;
- 26
وَٱلَّذِينَ يُصَدِّقُونَ بِيَوْمِ ٱلدِّينِ
Unukuzi: Wallazeena yusaddiqoona bi yawmid Deen
Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo,
- 27
وَٱلَّذِينَ هُم مِّنْ عَذَابِ رَبِّهِم مُّشْفِقُونَ
Unukuzi: Wallazeena hum min 'azaabi Rabbihim mushfiqoon
Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.
- 28
إِنَّ عَذَابَ رَبِّهِمْ غَيْرُ مَأْمُونٍۢ
Unukuzi: Inna 'azaaba Rabbihim ghairu maamoon
Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo.
- 29
وَٱلَّذِينَ هُمْ لِفُرُوجِهِمْ حَٰفِظُونَ
Unukuzi: Wallazeena hum lifuroo jihim haafizoon
Na ambao wanahifadhi tupu zao.
- 30
إِلَّا عَلَىٰٓ أَزْوَٰجِهِمْ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَٰنُهُمْ فَإِنَّهُمْ غَيْرُ مَلُومِينَ
Unukuzi: Illaa 'alaaa azwaajihim aw maa malakat aymaanuhum fainnahum ghairu maloomeen
Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi -
- 31
فَمَنِ ٱبْتَغَىٰ وَرَآءَ ذَٰلِكَ فَأُو۟لَٰٓئِكَ هُمُ ٱلْعَادُونَ
Unukuzi: Famanib taghaa waraaa'a zaalika fa ulaaa'ika humul 'aadoon
Lakini wanao taka kinyume ya haya, basi hao ndio wanao ruka mipaka.
- 32
وَٱلَّذِينَ هُمْ لِأَمَٰنَٰتِهِمْ وَعَهْدِهِمْ رَٰعُونَ
Unukuzi: Wallazeena hum li amaa naatihim wa 'ahdihim raa'oon
Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,
- 33
وَٱلَّذِينَ هُم بِشَهَٰدَٰتِهِمْ قَآئِمُونَ
Unukuzi: Wallazeena hum bishahaadaatihim qaaa'imoon
Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,
- 34
وَٱلَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ يُحَافِظُونَ
Unukuzi: Wallazeena hum 'alaa salaatihim yuhaafizoon
Na ambao wanazihifadhi Sala zao.
- 35
أُو۟لَٰٓئِكَ فِى جَنَّٰتٍۢ مُّكْرَمُونَ
Unukuzi: Ulaaa'ika fee jannaatim mukramoon
Hao ndio watakao hishimiwa Peponi.
- 36
فَمَالِ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ قِبَلَكَ مُهْطِعِينَ
Unukuzi: Famaa lil lazeena kafaroo qibalaka muhti'een
Wana nini wale walio kufuru wanakutumbulia macho tu?
- 37
عَنِ ٱلْيَمِينِ وَعَنِ ٱلشِّمَالِ عِزِينَ
Unukuzi: 'Anil yameeni wa 'anish shimaali 'izeen
Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto!
- 38
أَيَطْمَعُ كُلُّ ٱمْرِئٍۢ مِّنْهُمْ أَن يُدْخَلَ جَنَّةَ نَعِيمٍۢ
Unukuzi: Ayatma'u kullum ri'im minhum anyyudkhala jannata Na'eem
Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Pepo ya neema?
- 39
كَلَّآ ۖ إِنَّا خَلَقْنَٰهُم مِّمَّا يَعْلَمُونَ
Unukuzi: Kallaaa innaa khalaq nahum mimmaa ya'lamoon
La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanacho kijua.
- 40
فَلَآ أُقْسِمُ بِرَبِّ ٱلْمَشَٰرِقِ وَٱلْمَغَٰرِبِ إِنَّا لَقَٰدِرُونَ
Unukuzi: Falaaa uqsimu bi Rabbil mashaariqi wal maghaaribi innaa laqaadiroon
Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza
- 41
عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ خَيْرًۭا مِّنْهُمْ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ
Unukuzi: 'Alaaa an nubaddila khairam minhum wa maa Nahnu bimasbooqeen
Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi.
- 42
فَذَرْهُمْ يَخُوضُوا۟ وَيَلْعَبُوا۟ حَتَّىٰ يُلَٰقُوا۟ يَوْمَهُمُ ٱلَّذِى يُوعَدُونَ
Unukuzi: Fazarhum yakhoodoo wa yal'aboo hattaa yulaaqoo yaw mahumul lazee yoo'adoon
Basi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayo ahidiwa,
- 43
يَوْمَ يَخْرُجُونَ مِنَ ٱلْأَجْدَاثِ سِرَاعًۭا كَأَنَّهُمْ إِلَىٰ نُصُبٍۢ يُوفِضُونَ
Unukuzi: Yawma yakhrujoona minal ajdaasi siraa'an ka anna hum ilaa nusubiny yoofidoon
Siku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo,
- 44
خَٰشِعَةً أَبْصَٰرُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌۭ ۚ ذَٰلِكَ ٱلْيَوْمُ ٱلَّذِى كَانُوا۟ يُوعَدُونَ
Unukuzi: Khaashi'atan absaaruhum tarhaquhum zillah; zaalikal yawmul lazee kaanoo yoo'adoon
Macho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyo kuwa wakiahidiwa.
Toleo la tafsiri: sw.barwani
Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).
Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.
Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.