Sura zote

Surah 70

The Ascending Stairways

سُورَةُ المَعَارِجِ

Al-Ma'aarij · Makka

Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia

Sauti
  1. 1

    بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ سَأَلَ سَآئِلٌۢ بِعَذَابٍۢ وَاقِعٍۢ

    Unukuzi: Sa ala saaa'ilum bi'azaa binw-waaqi'

    Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea,

  2. 2

    لِّلْكَٰفِرِينَ لَيْسَ لَهُۥ دَافِعٌۭ

    Unukuzi: Lilkaafireen laisa lahoo daafi'

    Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia -

  3. 3

    مِّنَ ٱللَّهِ ذِى ٱلْمَعَارِجِ

    Unukuzi: Minal laahi zil ma'aarij

    Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.

  4. 4

    تَعْرُجُ ٱلْمَلَٰٓئِكَةُ وَٱلرُّوحُ إِلَيْهِ فِى يَوْمٍۢ كَانَ مِقْدَارُهُۥ خَمْسِينَ أَلْفَ سَنَةٍۢ

    Unukuzi: Ta'rujul malaaa'ikatu war Roohu ilaihi fee yawmin kaana miqdaaruhoo khamseena alfa sanah

    Malaika na Roho hupanda kwendea kwake katika siku ambayo kadiri yake ni miaka khamsini elfu!

  5. 5

    فَٱصْبِرْ صَبْرًۭا جَمِيلًا

    Unukuzi: Fasbir ssabran jameelaa

    Basi subiri kwa subira njema.

  6. 6

    إِنَّهُمْ يَرَوْنَهُۥ بَعِيدًۭا

    Unukuzi: Inaahum yarawnahoo ba'eedaa

    Hakika wao wanaiona iko mbali,

  7. 7

    وَنَرَىٰهُ قَرِيبًۭا

    Unukuzi: Wa naraahu qareebaa

    Na Sisi tunaiona iko karibu.

  8. 8

    يَوْمَ تَكُونُ ٱلسَّمَآءُ كَٱلْمُهْلِ

    Unukuzi: Yawma takoonus samaaa'u kalmuhl

    Siku ambayo mbingu zitakapo kuwa kama maadeni iliyo yayushwa.

  9. 9

    وَتَكُونُ ٱلْجِبَالُ كَٱلْعِهْنِ

    Unukuzi: Wa takoonul jibaalu kal'ihn

    Na milima itakuwa kama sufi.

  10. 10

    وَلَا يَسْـَٔلُ حَمِيمٌ حَمِيمًۭا

    Unukuzi: Wa laa yas'alu hameemun hameemaa

    Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake.

  11. 11

    يُبَصَّرُونَهُمْ ۚ يَوَدُّ ٱلْمُجْرِمُ لَوْ يَفْتَدِى مِنْ عَذَابِ يَوْمِئِذٍۭ بِبَنِيهِ

    Unukuzi: Yubassaroonahum; ya waddul mujrimu law yaftadee min 'azaabi yawma'izim bibaneeh

    Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe,

  12. 12

    وَصَٰحِبَتِهِۦ وَأَخِيهِ

    Unukuzi: Wa saahibatihee wa akheeh

    Na mkewe, na nduguye,

  13. 13

    وَفَصِيلَتِهِ ٱلَّتِى تُـْٔوِيهِ

    Unukuzi: Wa faseelathil latee tu'weeh

    Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu,

  14. 14

    وَمَن فِى ٱلْأَرْضِ جَمِيعًۭا ثُمَّ يُنجِيهِ

    Unukuzi: Wa man fil ardi jamee'an summa yunjeeh

    Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.

  15. 15

    كَلَّآ ۖ إِنَّهَا لَظَىٰ

    Unukuzi: Kallaa innahaa lazaa

    La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,

  16. 16

    نَزَّاعَةًۭ لِّلشَّوَىٰ

    Unukuzi: Nazzaa'atal lishshawaa

    Unao babua ngozi ya kichwa!

  17. 17

    تَدْعُوا۟ مَنْ أَدْبَرَ وَتَوَلَّىٰ

    Unukuzi: Tad'oo man adbara wa tawallaa

    Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka.

  18. 18

    وَجَمَعَ فَأَوْعَىٰٓ

    Unukuzi: W jama'a fa aw'aa

    Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi.

  19. 19

    ۞ إِنَّ ٱلْإِنسَٰنَ خُلِقَ هَلُوعًا

    Unukuzi: Innal insaana khuliqa haloo'aa

    Hakika mtu ameumbwa na papara.

  20. 20

    إِذَا مَسَّهُ ٱلشَّرُّ جَزُوعًۭا

    Unukuzi: Izaa massahush sharru jazoo'aa

    Inapo mgusa shari hupapatika.

  21. 21

    وَإِذَا مَسَّهُ ٱلْخَيْرُ مَنُوعًا

    Unukuzi: Wa izaa massahul khairu manoo'aa

    Na inapo mgusa kheri huizuilia.

  22. 22

    إِلَّا ٱلْمُصَلِّينَ

    Unukuzi: Illal musalleen

    Isipo kuwa wanao sali,

  23. 23

    ٱلَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ دَآئِمُونَ

    Unukuzi: Allazeena hum 'alaa Salaatihim daaa'imoon

    Ambao wanadumisha Sala zao,

  24. 24

    وَٱلَّذِينَ فِىٓ أَمْوَٰلِهِمْ حَقٌّۭ مَّعْلُومٌۭ

    Unukuzi: Wallazeena feee amwaalihim haqqum ma'loom

    Na ambao katika mali yao iko haki maalumu

  25. 25

    لِّلسَّآئِلِ وَٱلْمَحْرُومِ

    Unukuzi: Lissaaa 'ili walmahroom

    Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba;

  26. 26

    وَٱلَّذِينَ يُصَدِّقُونَ بِيَوْمِ ٱلدِّينِ

    Unukuzi: Wallazeena yusaddiqoona bi yawmid Deen

    Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo,

  27. 27

    وَٱلَّذِينَ هُم مِّنْ عَذَابِ رَبِّهِم مُّشْفِقُونَ

    Unukuzi: Wallazeena hum min 'azaabi Rabbihim mushfiqoon

    Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.

  28. 28

    إِنَّ عَذَابَ رَبِّهِمْ غَيْرُ مَأْمُونٍۢ

    Unukuzi: Inna 'azaaba Rabbihim ghairu maamoon

    Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo.

  29. 29

    وَٱلَّذِينَ هُمْ لِفُرُوجِهِمْ حَٰفِظُونَ

    Unukuzi: Wallazeena hum lifuroo jihim haafizoon

    Na ambao wanahifadhi tupu zao.

  30. 30

    إِلَّا عَلَىٰٓ أَزْوَٰجِهِمْ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَٰنُهُمْ فَإِنَّهُمْ غَيْرُ مَلُومِينَ

    Unukuzi: Illaa 'alaaa azwaajihim aw maa malakat aymaanuhum fainnahum ghairu maloomeen

    Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi -

  31. 31

    فَمَنِ ٱبْتَغَىٰ وَرَآءَ ذَٰلِكَ فَأُو۟لَٰٓئِكَ هُمُ ٱلْعَادُونَ

    Unukuzi: Famanib taghaa waraaa'a zaalika fa ulaaa'ika humul 'aadoon

    Lakini wanao taka kinyume ya haya, basi hao ndio wanao ruka mipaka.

  32. 32

    وَٱلَّذِينَ هُمْ لِأَمَٰنَٰتِهِمْ وَعَهْدِهِمْ رَٰعُونَ

    Unukuzi: Wallazeena hum li amaa naatihim wa 'ahdihim raa'oon

    Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,

  33. 33

    وَٱلَّذِينَ هُم بِشَهَٰدَٰتِهِمْ قَآئِمُونَ

    Unukuzi: Wallazeena hum bishahaadaatihim qaaa'imoon

    Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,

  34. 34

    وَٱلَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ يُحَافِظُونَ

    Unukuzi: Wallazeena hum 'alaa salaatihim yuhaafizoon

    Na ambao wanazihifadhi Sala zao.

  35. 35

    أُو۟لَٰٓئِكَ فِى جَنَّٰتٍۢ مُّكْرَمُونَ

    Unukuzi: Ulaaa'ika fee jannaatim mukramoon

    Hao ndio watakao hishimiwa Peponi.

  36. 36

    فَمَالِ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ قِبَلَكَ مُهْطِعِينَ

    Unukuzi: Famaa lil lazeena kafaroo qibalaka muhti'een

    Wana nini wale walio kufuru wanakutumbulia macho tu?

  37. 37

    عَنِ ٱلْيَمِينِ وَعَنِ ٱلشِّمَالِ عِزِينَ

    Unukuzi: 'Anil yameeni wa 'anish shimaali 'izeen

    Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto!

  38. 38

    أَيَطْمَعُ كُلُّ ٱمْرِئٍۢ مِّنْهُمْ أَن يُدْخَلَ جَنَّةَ نَعِيمٍۢ

    Unukuzi: Ayatma'u kullum ri'im minhum anyyudkhala jannata Na'eem

    Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Pepo ya neema?

  39. 39

    كَلَّآ ۖ إِنَّا خَلَقْنَٰهُم مِّمَّا يَعْلَمُونَ

    Unukuzi: Kallaaa innaa khalaq nahum mimmaa ya'lamoon

    La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanacho kijua.

  40. 40

    فَلَآ أُقْسِمُ بِرَبِّ ٱلْمَشَٰرِقِ وَٱلْمَغَٰرِبِ إِنَّا لَقَٰدِرُونَ

    Unukuzi: Falaaa uqsimu bi Rabbil mashaariqi wal maghaaribi innaa laqaadiroon

    Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza

  41. 41

    عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ خَيْرًۭا مِّنْهُمْ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ

    Unukuzi: 'Alaaa an nubaddila khairam minhum wa maa Nahnu bimasbooqeen

    Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi.

  42. 42

    فَذَرْهُمْ يَخُوضُوا۟ وَيَلْعَبُوا۟ حَتَّىٰ يُلَٰقُوا۟ يَوْمَهُمُ ٱلَّذِى يُوعَدُونَ

    Unukuzi: Fazarhum yakhoodoo wa yal'aboo hattaa yulaaqoo yaw mahumul lazee yoo'adoon

    Basi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayo ahidiwa,

  43. 43

    يَوْمَ يَخْرُجُونَ مِنَ ٱلْأَجْدَاثِ سِرَاعًۭا كَأَنَّهُمْ إِلَىٰ نُصُبٍۢ يُوفِضُونَ

    Unukuzi: Yawma yakhrujoona minal ajdaasi siraa'an ka anna hum ilaa nusubiny yoofidoon

    Siku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo,

  44. 44

    خَٰشِعَةً أَبْصَٰرُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌۭ ۚ ذَٰلِكَ ٱلْيَوْمُ ٱلَّذِى كَانُوا۟ يُوعَدُونَ

    Unukuzi: Khaashi'atan absaaruhum tarhaquhum zillah; zaalikal yawmul lazee kaanoo yoo'adoon

    Macho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyo kuwa wakiahidiwa.

Toleo la tafsiri: sw.barwani

Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).

Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.

Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.