Sura zote

Surah 1

The Opener

سُورَةُ ٱلْفَاتِحَةِ

Al-Faatiha · Makka

Katika surah hii, aya ya kwanza inajumuisha Basmalah; nambari za mistari ya kimataifa na uwekaji faharasa wa kawaida wa mushaf unaolingana.

Funguo: J ayah inayofuata · K ayah iliyotangulia

Sauti
  1. 1

    بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

    Unukuzi: Bismillaahir Rahmaanir Raheem

    KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

  2. 2

    ٱلْحَمْدُ لِلَّهِ رَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ

    Unukuzi: Alhamdu lillaahi Rabbil 'aalameen

    Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote;

  3. 3

    ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

    Unukuzi: Ar-Rahmaanir-Raheem

    Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu;

  4. 4

    مَٰلِكِ يَوْمِ ٱلدِّينِ

    Unukuzi: Maaliki Yawmid-Deen

    Mwenye Kumiliki Siku ya Malipo.

  5. 5

    إِيَّاكَ نَعْبُدُ وَإِيَّاكَ نَسْتَعِينُ

    Unukuzi: Iyyaaka na'budu wa lyyaaka nasta'een

    Wewe tu tunakuabudu, na Wewe tu tunakuomba msaada.

  6. 6

    ٱهْدِنَا ٱلصِّرَٰطَ ٱلْمُسْتَقِيمَ

    Unukuzi: Ihdinas-Siraatal-Mustaqeem

    Tuongoe njia iliyo nyooka,

  7. 7

    صِرَٰطَ ٱلَّذِينَ أَنْعَمْتَ عَلَيْهِمْ غَيْرِ ٱلْمَغْضُوبِ عَلَيْهِمْ وَلَا ٱلضَّآلِّينَ

    Unukuzi: Siraatal-lazeena an'amta 'alaihim ghayril-maghdoobi 'alaihim wa lad-daaalleen

    Njia ya ulio waneemesha, siyo ya walio kasirikiwa, wala walio potea.

Toleo la tafsiri: sw.barwani

Sauti ya aya: Mishary Rashid Alafasy (128kbps kupitia islamic.network CDN).

Maandishi na tafsiri: api.alquran.cloud · Uthmani Kiarabu.

Ikiwa maana ya aya haieleweki, muulize mwalimu aliyehitimu - hasa kwa masuala ya kisheria na imani.